LIVE STREAM ADS

Header Ads

SIKU YA TAKWIMU DUNIANI, WANANCHI WATAKIWA KUTOA TAKWIMU SAHIHI PINDI ZINAPOHITAJIKA.

Goodluck Lyimo ambae ni Meneja wa Takwimu Mkoa wa Mwanza na Geita akiwa Ofisini kwake baada ya kutembelewa hii leo na 99.4 Radio Metro na Mtanzaniamedia Blog.
Tanzania hii leo inaungana na Mataifa mbalimbali duniani katika Kuadhimishwa Siku ya Takwimu duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka Novemba 18, ambapo kitaifa siku hiyo inaaadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.

Akizungumza jana kuhusiana na Siku hii
Goodluck Lyimo ambae ni Meneja wa Takwimu Mkoa wa Mwanza na Geita, amebainisha kuwa siku hiyo ilitengwa mahususi kwa ajili ya kuhamasisha jamii na umma kwa pamoja kwa ajili ya matumizi ya takwimu, lengo likiwa ni kusaidia katika Mipango ya Kimaendeleo.

Alisema katika Maadhimisho ya Kitaifa yanayofanyika Jijini Dar es salaam mwaka huu, Machapicho mbalimbali yanayohusiana na Takwimu za Kitaifa zilizokusanywa katika maeneo mbalimbali yatatolewa kwa wananchi.

“Maadhimisho haya kwa sasa yanashindwa kuandimishwa katika ngazi ya Mikoa kutokana na ufinyu wa bajeti, japo malengo ya baadae ni kuhakikisha maadhimisho haya yanaadhimishwa hadi katika ngazi ya Mikoa”.Alibainisha Lyimo.

Katika hatua nyingine Lyimo aliongeza kuwa, mbali na Sensa ya Watu na Makazi ambayo hufanyika kila baada ya Miaka Kumi kwa ajili ya kutambua takwimu za watu na Makazi, pia Ofisi ya Taifa ya Takwimu hufanya tafiti zake mbalimbali ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa Takwimu za Mama na Mtoto lengo likiwa ni kubaini idadi ya idadi ya Watu lengo likiwa ni kusaidia katika shughuli za Maendeleo.

Hata hivyo Lyimo alibainisha kwamba bado kuna changamoto katika upatikanaji wa Takwimu hapa nchini, kwa kuwa wanajamii wengi kuanzia ngazi ya Kaya wamekuwa hawana desturi ya kutoa Twakimu zao sahihi.

Ametoa wito kwa wananchi kuwa tayari kutoa takwimu zao pindi zinapohitajika kwa kuwa Umhimu wa Takwimu ni kwa ajili ya mipango ya Kimaendeleo katika Taifa na si vinginevyo ambapo amewasihi baadhi ya wananchi ambao wamekuwa na desturi ya kuficha takwimu zao kuacha desturi hiyo.

Kauli mbiu katika Maadhimisho ya Siku ya Takwimu duniani Mwaka huu ni “Takwimu kwa Maendeleo, Tumia Takwimu kuliendeleza Taifa” ambapo imebainika kuwa ongezeko la idadi ya watu katika eneo husika husaidia kuchochea ukuaji wa Kimaendeleo katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuvutia wawekezaji.
Radio Metro Fm pamoja na Mtanzaniamedia Blog baada ya kutembelea Ofisi ya Takwimu Mkoa wa Mwanza.
Na:George Binagi.

No comments:

Powered by Blogger.