LIVE STREAM ADS

Header Ads

P-SQUARE WAKUBALI UWEZO WA DIAMOND.

Stori: Musa Mateja
MWACHENI Diamond aitwe Diamond! Hiyo kauli pekee unayoweza kuisema kufuatia wakali wa muziki wa R&B kutoka Nigeria, Peter na Paul Okoye ‘P-Square’
kuukubali uwezo wa kimuziki wa bwa’mdogo kutoka Tandale, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Bwa’mdogo kutoka Tandale, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa madansa wake ndani ya Lagos, Nigeria.
NI LAGOS, NIGERIA
Wakali hao walionesha kumpigia saluti Diamond baada ya kukutana naye kwenye tamasha la utoaji wa Tuzo za Wanamichezo Bora Afrika lililofanyika Lagos, Nigeria, usiku wa kuamkia Januari 9, mwaka huu.
WALIANZIA HOTELINI
Kwa mujibu wa chanzo kilichoambatana na Diamond nchini humo, saa chache kabla ya shoo kuanza, P-Square walimuibukia kwenye Hoteli ya Eko aliyofikia jijini humo na kummwagia pongezi nyingi sambamba na kumshauri baadhi ya vitu vya kimaendeleo.
‘Diamond Platnumz’ akifurahia jambo na Peter Okoye wa 'P Square'.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo hicho kilisema, P-Square walionekana kuvutiwa zaidi na juhudi binafsi za Diamond kiasi cha kuweza kuipeperusha bendera ya Afrika Mashariki katika levo za kimataifa.
“Jamaa walipomuona tu hotelini waliguswa sana na juhudi zake binafsi maana wanatambua jinsi gani muziki ulivyokuwa mgumu kuuvusha nje ya nchi yako lakini kwa kuwa Diamond ameweza, walimpigia saluti,” kilisema chanzo hicho.
ARUHUSIWA KOLABO
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data za ndani kwa kusema, mbali na kumpigia saluti, P-Square walionesha wako tayari kumsapoti Diamond kwa kumpa nafasi ya kufanya nao kazi yaani kolabo.
“Wamempa nafasi ya kufanya naye kazi pale atakapojisikia kutokana na mipango yake, kama akiamua kufanya sasa au baadaye ni uamuzi wake lakini jamaa (P-Square) hawana kinyongo naye lengo lao ni kuona muziki wa Afrika unateka dunia,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
‘Diamond Platnumz’ akiwa na Paul Okoye wa 'P Square'.
“Walimwambia the way (namna) alivyo na juhudi kwenye kazi yake anatambulika Nigeria utafikiri ni msanii kutoka Nigeria, walimpa mbinu zao za namna walivyopigana hadi kufika hapo walipo.”
Mbali na P-Square, mastaa mbalimbali wa Nigeria walimuibukia Diamond hotelini hapo akiwemo Mr Flavour na Jude Abaga ‘M.I’, ambao walimpa pongezi Diamond kwa kujua kumiliki vyema jukwaa kwani wamekuwa wakifuatilia shoo zake hasa anapotupia video zake mitandaoni.
Msanii wa muziki kutoka Nigeria, Mr Flavour akiteta jambo na 'Diamond Platnumz'.
APIGA SHOO YA MAANA
Ulipofika wakati wa kupanda jukwaani, Diamond aliitikisa Nigeria kwani alionesha vitu vya tofauti wakati akiimba nyimbo zake na kuwafanya Wanigeria na waalikwa mbalimbali wapigwe na butwaa huku wengi wakiishia kumpigia makofi na shangwe la kufa mtu.
DIAMOND ANASEMAJE?
Mwanahabari wetu alimcheki Diamond kupitia mtandao wa WhatsApp ambapo aliwashukuru mastaa hao wa Nigeria kwa upendo wao na kuahidi kuendelea kufanya maajabu zaidi katika levo za kimataifa.
“Wana wamenisapraizi hotelini, tumepiga stori nyingi, wameonesha wanakubali kile ambacho mimi nafanya, jukwaani nimefanya vizuri, watu na heshima zao mwishoni walipiga makofi kuonesha wamekubali.
Mkali wa Bongo Fleva kutoka Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz' akiwa na madansa wake.
KUHUSU KOLABO?
“Kuhusu kolabo na P-Square, ni mapema sana kuzungumzia kwa kuwa nina mipango mingi ya kufanya mwaka huu, mashabiki wakae mkao wa kula, nikiona inafaa, nitafanya nao maana wao hawana shida na mimi,” alisema Diamond.
P-SQUARE NI ZAIDI YA DAVIDO
Awali, kabla Diamond hajakutana na P-Square, alishirikiana na mkali mwingine wa Nigeria, Davido katika wimbo wake wa Number One Remix ambaye inaaminika kwa umaarufu na uwezo wa kimuziki yupo chini ya P-Square.
CREDIT: GLOBAL PUBLISHERS.

No comments:

Powered by Blogger.