LIVE STREAM ADS

Header Ads

AIRTEL YATOSHA ZAIDI, WASHINDI WATATU WAJISHINDIA MAGARI. BADO KUNA MAGARI 57. JIUNGE SASA.

Rebecca Mauma ambae ni Afisa Masoko Airtel Tanzania (Kushoto) akifuatiwa na Jane Matinde ambae ni Afisa Mahusiano Aiirtel Tanzania (Katikati) pamoja na Emmanuel Raphael ambae ni Afisa Masoko Kanda ya Ziwa wakizungumza hii leo na Wanahabari Jijini Mwanza ndani ya JB Belmont Hotel (Hawapo pichani) kuhusiana na Promosheni ya YATOSHA ZAIDI ambapo watumiaji wa vifurushi vya yatosha wanapata nafasi ya kujishindia zawadi nono ya Gari aina ya IST kila siku ndani ya siku 60.
Watanzania na Watumiaji wa Mtandao wa Simu wa Airtel wamehimizwa kuendelea kutumia vifurushi vya Airtel Yatosha Zaidi, ili kuingia katika droo ya kujishindia zawadi nono ya Gari aina ya IST.

Jane Matinde ambae ni Afisa Mahusiano Airtel Tanzania aliyasema hayo jana Jijini Mwanza, wakati akizungumza na Wanahabari kuhusiana na Promosheni hiyo ya Aitel Yatosha Zaidi ambayo inawawezesha watumiaji wa vifurushi vya Airtel Yatosha Zaidi pia kujipatia vifurushi vya Internet, SMS na dakika za kupiga kwenda mitandao yote ambapo vifurushi hivyo ni Vifurushi vya Siku, Wiki pamoja na Mwezi.

Alisema Promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi inamwezesha mtumiaji wa vifurushi vya Yatosha Zaidi hatimae kujishindia gari aina ya IST ambalo tayari limelipiwa kila kitu, ambapo kila siku mshindi mmoja atakuwa akipatikana huku promosheni hiyo ikidumu kwa muda wa siku 60 hivyo washindi 60 kila mmoja ataweza kujishindia gari ambapo unachotakiwa kufanya ni kupiga *149*99# ili kuweza kujiunga.

Baada ya Promosheni hiyo kuzinduliwa jumatatu ya wiki iliyopita, tayari watumiaji watatu wa Mtandao wa Simu wa Aitel wamejishindia Gari aina ya IST kila mmoja kupitia promoshoni hiyo ya Airtel Yatosha Zaidi inayoendeshwa na Kampuni ya Airtel Tanzania. Bado kuna magari 57 ya kushindaniwa ambapo kuna jumla ya magari ya 60 yatatolewa kwa washindi.

Washindi hao ni Namtapika Seif Kilumba (60) ambae ni mwalimu mstaafu kutoka Mkoani Mtwara, Ramadhan Mohamed Dilunga (53) mkulima kutoka Kimanzichana Mkoani Pwani pamoja na Mwajabu Omari Churian (27) ambae ni Mfanyabiashara  kutoka Mbagala Jijini Dar es salaam ambao wote waliibuka washindi na kujishindia  gari aina ya Toyota IST kila mmoja.

Emmanuel Raphael ambae ni Afisa Masoko Airtel Kanda ya Ziwa alibainisha kwamba tayari gari zinazoshindaniwa katika Promosheni hiyo ziko Jijini Mwanza na siku ya leo gari hizo aina ya IST zitakuwa zikizunguka katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza ambapo wateja wa Airtel watapata fursa ya kupiga picha katika magari hayo huku wakipata huduma mbalimbali za Airtel.

Nae Rebecca Mauma ambe ni Afisa Masoko Airtel Tanzania aliwakumbusha wateja na watumiaji wa Airtel kuwa pindi mshindi wa Promosheni ya Yatosha Zaidi anapopatikana anapigiwa simu kwa nambari 0684 29 11 05 hivyo wawe makini na baadhi ya watu wenye nia mbaya ambao wanaweza kutumia fursa hii kwa njia ya utapeli.
Rebecca Mauma ambae ni Afisa Masoko Airtel Tanzania (Kushoto) akifuatiwa na Jane Matinde ambae ni Afisa Mahusiano Aiirtel Tanzania (Katikati) pamoja na Emmanuel Raphael ambae ni Afisa Masoko Kanda ya Ziwa wakizungumza hii leo na Wanahabari Jijini Mwanza ndani ya JB Belmont Hotel (Hawapo pichani) kuhusiana na Promosheni ya YATOSHA ZAIDI ambapo watumiaji wa vifurushi vya yatosha wanapata nafasi ya kujishindia zawadi nono ya Gari aina ya IST kila siku ndani ya siku 60.
Rebecca Mauma ambae ni Afisa Masoko Airtel Tanzania (Kushoto) akifuatiwa na Jane Matinde ambae ni Afisa Mahusiano Aiirtel Tanzania (Katikati) pamoja na Emmanuel Raphael ambae ni Afisa Masoko Kanda ya Ziwa wakizungumza hii leo na Wanahabari Jijini Mwanza ndani ya JB Belmont Hotel (Hawapo pichani) kuhusiana na Promosheni ya YATOSHA ZAIDI ambapo watumiaji wa vifurushi vya yatosha wanapata nafasi ya kujishindia zawadi nono ya Gari aina ya IST kila siku ndani ya siku 60.
Rebecca Mauma ambae ni Afisa Masoko Airtel Tanzania (Kushoto) akifuatiwa na Jane Matinde ambae ni Afisa Mahusiano Aiirtel Tanzania (Katikati) pamoja na Emmanuel Raphael ambae ni Afisa Masoko Kanda ya Ziwa wakizungumza hii leo na Wanahabari Jijini Mwanza ndani ya JB Belmont Hotel kuhusiana na Promosheni ya YATOSHA ZAIDI ambapo watumiaji wa vifurushi vya yatosha wanapata nafasi ya kujishindia zawadi nono ya Gari aina ya IST kila siku ndani ya siku 60.
Wanahabari/ Watangazaji Radio Free Africa.
Wanahabari na Wadau wa Airtel.
Wanahabari/ Watangazaji Radio Metro Fm.
Wanahabari/ Watangazaji Radio Free Africa Kiss Fm.
Na: George Binagi-GB Pazzo.

No comments:

Powered by Blogger.