LIVE STREAM ADS

Header Ads

PUMZIKA KWA AMANI KAPTENI KOMBA. WATANZANIA WATAKUKUMBUKA NA HII KAULI YAKO.

Na:George Binagi-GB Pazzo
Mbunge wa Mbinga Magharibi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Kapteni John Damian Komba amefariki dunia hii leo akiwa katika Hospitali ya TMJ Jijini Dar es salaam ambapo chanzo cha kifo chake kimeelezwa kuwa ni kutokana na tatizo la kisukari alilokuwa nalo.

Mbali ya kuwa mwanasiasa pia Komba ndiye aliyekuwa kiongozi wa kundi la TOT sanjari na kuwa msanii aliekuwa akiimba kwaya katika kundi hilo ambalo lilijumuisha sanaa mbalimbali zikiwemo kwaya, dansi, sarakazi pamoja na taarabu.

Kapteini Komba ambae pia alikuwa ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM miongoni mwa kauli zake zitakazokumbukwa ni pamoja na kauli yake aliyoitoa enzi za uhai wake wakati akihojiwa katika kipindi cha Mkasi Tv kinachoruka EATv ambapo alipoulizwa ni mwanasiasa gani anastahili kuwa rais wa Tanzania kupitia chama chake cha CCM alisema kuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh.Edwan Lowasa anafaa kuwa rais.

‘’...Mimi hapa nilipo leo ukiniuliza nani anafaa kuwa rais, mimi nasema Lowasa anafaa kuwa rais kamili eeeeeh nitasema Edwad Lowasa anafaa kuwa rais kabisa. Kama chama changu kitampendekeza mimi mia kwa mia kabisa...’’.


Pumzika kwa Amani Kapteini Komba lakini umeondoka katika kipindi ambacho pengine ulitakiwa kusalia hapa duniani ili kuweza kushuhudia na kujionea kauli uliyoitoa juu ya nani anastahi kuwa rais wa Tanzania kupitia chama chako cha CCM kama ingeweza kutimia kuwa kweli ama la!

No comments:

Powered by Blogger.