Badrudini Nsubuga (wa tatu pande zote) ambae ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi ya Marehemu Kosha Marsh akitoa ratiba kamili ya Msiba wa Marehemu Marsh wakati akizungumza na Metro Fm & Binagi Media Group.
Wakizungumza kwa masikitiko Makubwa baadhi ya wadau wa michezo Jijini Mwanza wameeleza kusikitishwa kwa kitendo cha mwili wa Marehemu Mwalimu Marsh kusafirishwa kwa njia ya barabara (Kwa gari/ Coaster) kutoka Jijini Dar es salaam hadi Jijini Mwanza ukilinganisha nafasi aliyokuwa nayo katika Soka la Tanzania.
Wameongeza kuwa wamesikitishwa namna Chama cha Soka Mkoani Mwanza MZFA pamoja na Shirikisho la Soka nchini TFF walivyoshindwa kumuenzi Marehemu Mwalimu Marsh hususani kwa namna mwili wake ulivyosafirishwa sanjari na katika michezo ya ligi kuu ya Tanzania bara iliyochezwa jana kushindwa kuonyesha ishara ya aina yoyote ya kumuenzi marehemu Marsh.
|
tumesikitika kuondokewa na mtaalam huyu wa soka......lakini pia ni muhimu wadau wote wa soka hasa wachezaji kuandaa maisha yao ya baadaye ili kuondokana na utegemezi wa misaada wakati wa matatizo ya kuugua na misiba...
ReplyDelete