LIVE STREAM ADS

Header Ads

UCHAMBUZI: UBINGWA LIGI KUU ENGLAND (EPL) UKO WAZI KWA CHELSEA.

0713208878
Ni siku chache zilizopita kwa wapenda soka  ulimwengu kushuhudia mechi kati ya Chelsea na Man united Binagi Media Group inakuletea kumbukumbu muhimu juu ya mechi hiyo.

Hii ni mechi ambayo ilipigwa katika dimba la Staford Bridge kama ambavyo mashabiki wa Chelsea wamekuwa wakiita uwanja huo kwa jina la Darajani ikiwa ni mechi ambayo ilitarajiwa kuwa na upinzani mkubwa na mvuto wa aina yake lakin haikuwa hivyo.

Kwa upande wa Chelsea ilikuwa ni mechi ya 701 tangu inunuliwe na tajiri wa timu hiyo Roman Abramovich mwaka 2000 ambaye ametumia paund million 916.95 kwa kipindi chote hicho.

Mechi hiyo ilichezwa majira ya saa 1.30 usiku kwa saa zaAfrika Mashariki na zifuatazo ni takwimu za mechi 10 zilizopita kati ya Chelsea na Man United.
2014/2015 Man united 1-1 Chelsea premier
2013/2014 Chelsea fc  3-1 Man unit premier
2012/2013 Man unit 0- 0   Chelsea premier
2012/2013 Man unit 0- 1 Chelsea  premier
2012/2013 Chelsea 5-4 Man unit league cup
2012/2013 Chelsea 2-3 Man unit premier
2011/2012 Chelsea 3-3 Man unit premier
2011/2012 Man unit 3-1 Chelsea premier
2010/2011 Man unit 2-1 Chelsea premier
2010/2011 Man unit 2-1 Chelsea ligi ya mabingwa

Mechi 10 zilizopita
Man unit kashinda 4
Chelsea fc kashinda 3
Zote zimetoka Sare mara 3
MECHI ZA JUMLA
Chelsea kashinda 46
Man unit kashinda 68
Zimetoka Sare 50

Hizo ndizo takwim za timu hizi mbili ni mechi ambayo ilitakuwa na upinzani wa aina yake kwani kwa kila timu point 3zilikuwa  ni muhimu kwake japo kwa sasa Chelsea iko kileleni mwa ligi ikiwa na point 76 ikiwa imecheza michezo 32 huku Man United ikiwa nafas ya 3 na pointi zake 65 baada ya kushuka dimbani mara 33.

Nafasi ya 2 inashikiliwa na Asernal na point 66 akiwa amecheza michezo 32 hata hivyo mambo yamebadilika baada ya timu za asernal na man united kuzinduka toka usingizin na kuingia kwenye kundi la kupigania ubingwa huku tukishuhudia Man City ikianza kupotea.

Kwa hali hii Chelsea anapewa nafasi ya kuchukua ubingwa hivyo Mourinho hakuhitaji kucheza mchezo wa pasi bali alicheza mchezo wa kupaki basi hivyo alichokuwa akiangalia ni point na siyo  kucheza mchezo ambao  ni show game kwan point 3 ni zilikuwa ni  muhimu kwake na ndicho kitu alichokifanya huku akiwa anajua kuwa ana kibarua kigum kwan mechi inayofuata ambapo atakuwa mdomon mwa Asernal.

Lakin tukumbuke kuwa Mourinho ameishaweka kombe la Capital one kabatini.Ni kwa nini nasema kuwa Chelsea alicheza mchezo mchafu usiyokuwa na radha hilo lilionekana mapema toka siku  Chelsea alipocheza mechi na QPR na Chelsea aliibuka na ushindi wa goli 1-0  ambapo wasiwasi wangu mkubwa kabla ya mechi hii ulikuwa  ni kwa mabeki wa Man united ambao hata kwenye mechi ya man United na Man City mabeki wa United walionekana kupwaya sana hususani katika kipindi cha kwanza na kuwapatia nafasi mafowadi wa City kupata nafasi lakini hawakuwa makini kutumia nafasi hizo.

Mechi hiyo ilionekana kuwa   ngumu kwa viungo wa Man united kutokana na Chelsea kupaki basi katikati ya uwanja nikiwa namaanisha viungo ndo wangeweza kuamua mchezo huo ila mwisho wa siku Chelsea iliibuka na ushindi ambao ulikuwa ni muhimu kwao  sare  kwani hatamimi sikutarajia kama  United ingeibuka   na ushindi darajani.Kwenye mchezo huo goli la Eden Hazard dakika ya 38 lilitosha kuipa ushindi Chelsea licha ya Ushindi huo Man united walitawala mchezo mpaka dakika 90 walikuwa wanaongoza umiliki wa mpira kwa 71% Kwa 19% za Chelsea.

Hata hivyo timu mbili hazikuwa na makeke ya kutosha na kila moja ilipiga  mashuti mawili tu yaliyolenga lango kwa dakika zote 90.Mashuti ambayo hayakulenga langoMan walipiga mashuti9 dhidi ya 3 ya Chelsea; United ilipata kona 7 dhidi 3 zaChelsea lakini United hawakukwepa kipigo toka kwa vinarahao wa ligi kuu England hata hivyo ushindi huo umeifanya Chelsea kuwa mbele kw point kumi dhidi ya mshindi wa pili ambaye ni Arsenal mwenye pointi 66

HIZI NI MECHI 6 ZILIZOBAKI CHELSEA KUWA BINGWA WA EPL 2014/2015.
Zimebaki mechi sita kwa Chelsea ili watangazwe kuwa mabingwa wa msimu wa mwaka 2014/2015hadi kufikia tarehe 24 mwezi wa5 ndo tarehe ambayo tutakuwa tumejuwa bingwa ni nani  mechi hizo ni;
Asrsenal Vs Chelsea [jumapili 26 /4]
LeicesterCity Vs Chelsea [jumatano 29/4]
Chelsea Vs Ceystal Palace[jumapili 3/5]
Chelsea Vs Liverpool[jumapili 10/5]
West Brownwich Abion Vs Chelsea [18/5]

Chelsea Vs Sundeland [24/4]

Kwa hali ilivyo ni matarajio ya wanamichezo wengi hata nami nikiwemo ya kwamba ni ukweli usiopingika kuwa Chelsea ndie bingwa wa Ligi Kuu Nchini Englind kwa Msimu wa mwaka 2014/15.
                                       CREDIT:RADIO METRO

No comments:

Powered by Blogger.