KAULI YA MWAKYEMBE BUNGENI MJINI DODOMA YALETA FARAJA KWA WATUMIAJI WA SIMU NCHINI.
Anaezungumza ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Harison Mwakyembe (Picha kutoka Maktaba).
ELISA ANATORY 0763345064
EMAIL
anatoryelisa@gmail.com
Waziri
wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Harison Mwakyembe amesema kuwa nchi wanachama
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimefikia
makubaliano kuhusu kupunguza gharama za
huduma za simu za kimataifa ili kuweka mfumo bora wa mawasiliano baina ya nchi
hizo.
Mwakyembe aliyasema hayo hii leo bungeni mjini Dodoma wakati akiwasilisha
makadilio ya mapato ya wizara yake.
Alisema kuwa nchi hizo wanachama zamekubaliana kushushwa kwa
gharama hizo na kuwa dola za Kimarekani 0.7 kwa dakika moja kwa watoa huduma,
na dola za kimarekani 0.1kwa dakika kwa watumiaji wa kawaida.
Waziri Mwakyembe aliongeza kuwa nchi hizo zimekubaliana pia
kuondoa gharama kwa mpokeaji wa simu iliyounganishwa miongoni mwa nchi wanachama
wa jumuiya hiyo ambapo alibainisha kwawa viwango hivyo vitaanza kutumika
kuanzia mwaka wa fedha wa 2015/2016.
Kuhusu miundombinu ya
barabara, Mwakyembe alisema kuwa serikali imekamilisha ujenzi wa daraja la
kimataifa la Lusumo lililopo mpakani mwa Tanzania na Rwanda lenye uwezo wa
kupitisha magari manne yenye uzito wa tani 54 kila moja tofauti na magari
mawili yaliyokuwa yakipita katika daraja
hilo hapo awali na hivyo kusababisha adha kubwa ya usafilishaji.
No comments: