LIVE STREAM ADS

Header Ads

PLUIJM ATANGAZAKIKOSI CHA MAUAJI YA ETOILE DU SAHILE YA TUNISIA.

Picha Kutoka Maktaba
Na:Genya Richard
Kocha Timu ya Yanga Mhoholanzi Hans der Pluijm ametangaza kikosi kitakachowavaa Watunisia hii leo jumamosi May 2 mwaka 2015 katika Michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika ambapo timu hiyo inachuana na Etoile Du Sahile.

Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa kuanzia majira ya saa 01:00 jioni kwa saa za Afrika ya Kaskazin huku kwa saa za Afrika Mashariki ikiwa ni saa 3.00 za jioni ambapo mechi hiyo inatarajiwa na kituo cha Azam 2 cha hapa nchini.

Timu ya Yanga Hans der PLUIJM amewataja wachezaji watakakipiga katika mechi hiyo kuwa ni;
1.Ally Mustapha
2.Mbuyu Twite
3.Osca Joshua
4.Kelvin Yondani
5.Nadir Haroub
6.Said Makapu
7.Saimon Msuva
8.Salum Telela
9.Hamisi Tambwe
10..Mrisho Ngassa
11.Pah Sherman

Hicho ndicho kikosi cha kwanza cha Yanga kinachotarajiwa kupambana na Etoile du Sahel ambapo itakumbukwa kuwa katika Mechi ya Kwanza hapa nchini timu hizo zilitoka suluhu ya 1-1, matokeo ambayo yanailazimu yanga kusaka ushindi ugenini na si vinginevyo ili iweze kusonga mbele katika michuano hiyo ya Klabu bingwa barani Afrika.


Je una maoni yoyote kuhusu kikosi hicho? unafikri kuna sehemu ya kufanyia marekebisho ili Yanga ifanikiwe kupata ushindi? Toa maoni yako kupitia 0713208878

No comments:

Powered by Blogger.