LIVE STREAM ADS

Header Ads

KOTECHA AWAHIMIZA WANANCHI JIJINI MWANZA KUWA WATUNZAJI BORA WA MAZINGIRA.

Diwani wa Kata ya Nyamagana Jijini Mwanza Bhikhu Kotecha (Katikati) akizungumza katika Kilele cha Wiki ya Mazingira Jijini Mwanza hii leo. Kushoto ni Afisa Mazingira Jiji la Mwanza Charles Amani na Kulia ni Mrashy Diana Manyilizo ambae ni Mwenyekiti wa Asasi ya Uchungu na Mwana Mkoani Mwanza.
 Na:Malongo Mbeho
Wananchi wa jiji la Mwanza waehimizwa kutunza mazingira na kulinda vyanzo vya maji ili kujiepusha na magonjwa ya milipuko.

Bhikhu Kotecha ambae ni diwani wa Kata ya Nyamagana Wilayani Nyamagana alitoa ushauri huo hii leo katika kilele cha maadhimisho ya wiki yamazingira duniani yaliyoadhimishwa katika bustani ya TAMPERE iliyopo eneo la Makongoro Jijini Mwanza.

Kotecha alisema kuwa uhifadhi wa maji, ardhi na hewa hutasaidia usalama wa afya ya binadamu na na hivyo kupunguza magonjwa hatarishi kama vile  kipindupindu na kuhara husababishwa na utunzaji mbovu wa mazingira.

Nae Charles Amani ambae ni afisa mazingira Jiji la Mwanza aliwahimiza wananchi kuwa na desturi ya kutunza mazingira kwa kushirikiana na ofisi za mazingira zilizopo katika maeneo yao

Amani alisema kuwa elimu ya utunzaji wa mazingira inaendelea kutolewa kwa wananchi lengo likiwa ni kila mmoja kutambua wa uhufadhi wa mazingira.


Wiki ya Mazingira Duniani ilianza kuanzimishwa tangu June Mosi mwaka huu na kilele chake kikiwa ni hii leo juni tano ambapo kitaifa maadhimisho hayo yamefanyiki mkoani Tanga kwa kauli mbiu isemayo NDOTO BILIONI SABA DUNIA MOJA, TUMIA RASILIMALI KWA UANGALIFU kikiwa kimelenga kuwahimiza wananchi kutumia rasilimali zilizopo kunendana na idadi ya watu iliyopo.
Kulia ni Afisa Mazingira Jiji la Mwanza Charles Amani na Kulia ni Mrashy Diana Manyilizo ambae ni Mwenyekiti wa Asasi ya Uchungu na Mwana Mkoani Mwanza akizungumza kwa niaba ya asasi zisizo za Serikali Mkoani Mwanza. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Nyamagana Jijini Mwanza Bhikhu Kotecha.
Maoni kutoka kwa wadau wa Mazingira yalitolewa pia
Maoni kutoka kwa wadau wa mazingira yakitolewa
Mazingira ni uhai
Wanafunzi nao walishirikishwa juu ya namna ya utunzaji wa mazingira ambapo pia walipata fursa ya kutoa maoni yao
Wadau wa Mazingira Mkoani Mwanza
Kilele cha Wiki ya Mazingira Jijini Mwanza
Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Jijini Mwanza
SOMA BANGO HILO KWA UMAKINI.
KUONA SIKU YA UFUNGUZI BONYEZA HAPA
KUTAZAMA ILIVYOKUWA MWAKA JANA BONYEZA HAPA

No comments:

Powered by Blogger.