TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KATIKA SIKU YA KUPIGA VITA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA.
Katikati ni Edwin Soko ambae ni Mwenyekiti wa OJADACT akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari hii leo juu ya Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya Duniani yanayotarajiwa kufanyika Kesho. Kulia ni Neema Joseph ambae ni Mhasibu wa OJADACT na Kushoto ni Isaack Wakuganda ambae ni Afisa Jinsi OJADACT.
Chama
cha waandishi wa habari wa
kupiga vita matumizi
ya dawa za kulevya
na uhalifu Tanzania (ojadact)
leo tunafanya mkutano na nyinyi ikiwa
maudhui makubwa ni kampeni
zetu kuelekea kwenye maadhimisho ya kidunia
ya kupiga vita matumizi
ya dawa za kulevya duniani, juni 26, 2015.
Ndugu
waandishi wa habari maadhimisho
ya mwaka huu kitaifa
yatafanyika mkoani pwani wilaya
ya bagamoyo, na kimkoa
yatafanyika eneo la
igogo . Kauli mbiu ya
mwaka huu itakuwa
ni, jenga jamii, maisha na
utu bila dawa za kulevya.
Hali
ya dawa za kulevya kitaifa:
Ndugu
waandishi licha ya
kuadhimisha kila mwaka
siku ya kupiga
vita matumizi ya
dawa za kulevya duniani tatizo
la dawa za
kulevya limeendelea kuwa kubwa kiasi
cha kutia shaka, tuna
imani juhudi kubwa
zinahitajika za kupambana
na dawa za kulevya.
Kitakwimu ripoti mpya ya ofisi ya umoja wa mataifa ya
kupambana na mihadarati na uhalifu (unodc), imesema tanzania ni kinara wa
kupitisha dawa za kulevya katika nchi za afrika mashariki. Ripoti hiyo, imesema
jumla ya tani 64 za dawa za kulevya aina ya heroine, zilisafirishwa bila
kukamatwa kwenda au kupitia afrika mashariki, ikiwemo tanzania kati ya mwaka
2010 na 2013.
Ripoti hiyo, imesema nchini tanzania
mji wa tanga, ndio kinara na njia kuu ya kusafirishia dawa hizo kwani tangu
mwaka 2010, ukamataji uliongezeka kutoka kilo 145 hadi kilo 813 mwaka huu.
Wastani wa ukamataji wa shehena za
dawa za kulevya eneo hilo, uko katika kilogramu 1,011 mwaka 2013 kutoka 145
kilo za awali.
Takwimu zinaonyesha kwa pamoja
watanzania na wakenya, wanaongoza kwa utumiaji na usafirishaji dawa za kulevya
aina ya cocaine, huku wakitumia dola milioni 160 kila mwaka. Lakini katika
kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kati ya mwaka 2010 na 2013, shehena
zilizokamatwa na maofisa husika nchini tanzania, kenya, shelisheli na
mauritius zilikuwa tani 1.6
Hali
ya matumizi ya
dawa za kulevya Mkoa wa Mwanza.
Mkoa wa Mwanza unakadiliwa kuwa na watumiaji wa dawa za kulevya wapatao 10,000 kwa mujibu wa takwimu za mganga
mkuu wa mkoa wa mwanza.
Kwa
mujibu wa tafiti ya tume
iliyofanywa Mwanza, wilaya ya
nyamagana na ilemela hadi
kufikia agosti, 2014 ilikuwa na
watumiaji wa dawa za kulevya wapatao 3,300, kati yao
wanaojidunga walikuwa 300.
Pia kwa mujibu wa shirika
la icap hadi
kufikia mei, 2015 watumiaji wa dawa 1093 walijitokeza
kupima ukimwi ili kujua
afya zao.
Mtazamo
wa Chama(OJADACT)
Licha
ya tatizo la dawa
za kulevya kuendelea kuwa
kubwa, hakuna jitihada za
dhati zinazolingana na
ukubwa wa tatizo
zilizoonyeshwa na serikali
pamoja na Taifa
kwa ujumla ili
kukabiliana na hali iliyopo.
Kumekuwa na
uzembe wa makusudi wa kutaja
nafasi ya Nchi
kimataifa juu ya
tatizo la dawa
za kulevya na badala yake
serikali imekuwa ikificha uhalisia
wa tatizo.
Tafiti na ripoti za
kimataifa ndizo pekee
zimekuwa zikionyesha ukweli
juu ya tatizo
la dawa za kulevya kimataifa.
Rai
yetu kwa Nchi
•Vita dhidi
ya dawa za kulevya
zinahitaji nguvu za pamoja ili
kukomesha biashara hiyo
•Serikali
na taasisi mbalimbali
zijikite katika kutoa
elimu ya kutosha
juu ya dawa za kulevya.
•Upatikanaji wa
sera ya dawa
za kulevya uharakishe ili
kusaidia kumaliza tatizo
•Sheria mpya
ya dawa za kulevya ya
mwaka 2014 isimamiwe na
kutekelezwa ili kuleta tija kwa Taifa
•Vita dhidi
ya dawa za kulevya zitangazwe
kuwa janga la kitaifa
•Moja ya
sifa za Rais ajaye
iwe ni kuwa na uwezo wa kukabiliana na
biashara ya dawa za kulevya kama
alivyofanya Rais Richard
Nickson wa Marekani
•Serikali iweke
wazi ukubwa wa tatizo la dawa za kulevya ili
Taifa liweze kujitathimini na kutafuta
njia mbadala ya
kumaliza tatizo.
Ushiriki wa maadhimisho
Ndugu waandishi wa habari maadhimisho
ya mwaka huu kitaifa yatafanyika
Mkoa wa Pwani , wilaya ya
Bagamoyo, ambako OJADACT
tutashiriki na kimkoa yatafanyika
kata ya Igogo, hivyo
basi tunawaomba waandishi
wote kushiriki kikamilifu kwenye
maadhimisho hayo yenye
kauli mbiu, JENGA JAMII, MAISHA NA UTU
BILA DAWA ZA KULEVYA.
Salamu
toka kwa Katibu Mkuu wa
Umoja wa mataifa.
Kila
mtu ajitathimini kuwa ametimiza
jukumu lake la kuilinda
jamii dhidi ya
janga la dawa za kulevya.
Nawashukuru sana ndugu waandishi wa habari.
Edwin
soko
Mwenyekiti
OJADACT.
Neema Joseph (Kulia) ambae ni Mhasibu wa OJADACT akitoa ufafanuzi juu ya Maadhimisho ya Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya yanayotarajiwa kufanyika Kesho. Kushoto ni Edwin Soko ambae ni Mwenyekiti wa OJADACT.
Wanahabari Mkoani Mwanza
Wanahabari Mwanza
No comments: