LIVE STREAM ADS

Header Ads

TOTO AFRICAN YA JIJINI MWANZA KUTUMIA SHILINGI MILIONI 495 KATIKA MSIMU UJAO WA LIGI KUU.

N:Oscar Mihayo
Klabu ya Toto African ya Jijini Mwanza  imetenga kiasi cha Sh.495 Milioni kwa ajili ya Bajeti ya msimu ujao wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ikiwa ni moja ya mipango yake ya kuhakikisha inafanya vizuri na kuwa tishio ya vigogo wa ligi hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano mkuu wa Klabu hiyo uliofanyika juzi Jijini Mwanza, Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo Ahmed Waziri Gao alisema kuwa kutokana na ushindani uliopo kwa vilabu vya ligi kuu, kamati tendaji ya timu hiyo imetenga kiasi hicho cha fedha ambacho kitaweza kutumika kwa ajili ya msimu ujao.

“Kuna ugumu na ushindani wa ligi kuu kwani vilabu vimejipanga Kwa hiyo na sisi kama kamati tendaji tumepanga kutumia kiasi cha Sh.495 ambacho kitaweza kutumika kwenye msimu ujao lengo likiwa ni kutusaidia kupata ubingwa na si kushiriki tu”. Alisema Gao.

Bajeti hiyo iliungwa mkono na wanachama waliohudhuria mkutano huo ambapo walisema kuwa huu ni muda muafaka wa maandalizi ya Klabu hiyo, hivyo bajeti hiyo itasaidia kuinua timu yao.

Akifafanua matumizi ya fedha hizo Katibu Mkuu wa Klabu hiyo Ernest Shija Mpiwa alisema kuwa Usajili utagharimu kiasi cha shilingi Milioni 30,Mishahara milioni 138 na Safari milioni 40.

Nyingine ni Kambi shilingi milioni 165, Uhamisho Milioni sita, Vifaa tiba milioni mbili huku Uendeshaji wa timu hiyo pamoja na ile ya vijana wenye umri chini ya miaka 18 zikitengwa shilingi Milioni 145.

Katibu huyo alisema kuwa bajeti hiyo itasaidia kubadilisha hali ya Klabu na mazingira kwa ujumla na hivyo kuweza kuifanya timu ya Toto kufanya vizuri katika msimu ujao wa ligi.

“Hii bajeti tuna matumaini itatuweka katika hali nzuri ikiwa ni pamoja na kubadilisha hali na mazingira ya Klabu hivyo kupitishwa kwake ni mafanikio kwa timu yetu.”Alisema Mpiwa.


Aidha mmoja wa wanachama wa klabu hiyo Kabuka Magalula aliomba kamati ya usajiri kusajili kujikiza zaidi katika kusajili wachezaji wazawa na kuachana na wachezaji walioachwa na timu kubwa kama Simba na Yanga kwani huo utakuwa ndio mwisho wa hujuma za wacheza kutoka klabu hizo kubwa hapa nchini.

No comments:

Powered by Blogger.