LIVE STREAM ADS

Header Ads

MAKALA FUPI: NJIA BORA ZA KUULINDA MTAJI WA BIASHARA YAKO.

Mwandishi wa Makala hii Edwin Soko (Aliesimama)ni Mwenyekiti wa Chama cha Wajasiriamali Tanzania, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uharifu nchini Tanzania akiwa pia ni Mratibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mwanza.
Na:Edwin Soko
Simu:0754 551 306
Ndugu msomaji imekuwa kawaida sana kusikia  wanadamu kila kukicha wakiweka mipango ya  usalama wa maisha yao, kama kuwa na afya  bora, usalama wa maisha yao kwa kuwa na nyumba yenye ulinzi, gari lisilo na matatizo, lakini imekuwa vigumu sana kusikia  wajasiriamali wakijadili usalama wa mitaji yao.

Hali  hii  imekuwa  ikiwasababishia wengi wao maumivu makubwa hasa baada ya kupoteza mitaji yao, kwa kuwa tu walishindwa kuilinda kwa kujua njia bora za kulinda mitaji ya bishara zao.

Nimeona ni vyema kuleta makala hii yenye  kutoa elimu ya namna ya kulinda mtaji wa bishara yako, muda mfupi uliopita  niliwasilisha maudhui haya kwenye kituo cha  redio cha Metro Fm klichopo Jijini Mwanza.

Lakini nikaguswa pia kuandika katika fasihi  andishi ili kazi hii iweze kuishi milele na milele na kusomwa na watu wengi, ambapo  naamini italeta mageuzi makubwa katika  ubongo wa Wasomaji wake.

Zifuatazo ni njia bora za kulinda mtaji wa  bishara yako, ungana nami katika ukurasa huu.

Njia  ya  kwanza; ni kutunza kumbukumbu za  bishara yako, jenga desturi ya kuweka  kumbukumbu za mauzo ya bishara yako kila  siku, hii itakusaidia kutathimini bishara yako na hatimaye kujua mwenendo wa bishara  yako. 

Watu wengi weliofanikiwa kama Bill  Gates, Mengi na wengineo wamekuwa na utaratibu mzuri wa kutunza kumbukumbu za  bishara zao.

Njia  ya  pili; ni kutenganisha biashara  yako na urafiki hasi, epuka kuwa na marafiki walio na ajenda ya kunufaika kupitia   urafiki wako, kwani moja ya matokeo yake ni  kukuingiza kwenye mitego ya kiuchumi ili na wao waweze kupata chochote. 

Kuna mfano hai  wa rafiki yangu mmoja alijikuta anafirisika baada ya kupata ushauri mbaya wenye manufaa kwa rafiki yake baada ya kushauriwa anunue gari la kutembelea ili wawe wanatoka Out wikiendi badala ya kujenga nyumba ya bishara na kuikuza zaidi.

Njia ya  tatu; Ni wekeza faida unayoipata  katika bishara ya kwanza kwenye biashara ya pili na hata ya tatu na kuendelea ili  izalishe zaida maradufu na kukusaidia kuzidi kupata faida kubwa inayoweza kukusaidia kufanya kitu kingine kikubwa kwa mara moja, kama kujenga nyumba au kufungua duka. 

Hapa natoa angalizo, kuna wafanyabishara  wengi wanatumia faida kwa mambo yasiyo ya  kimsingi kama kulewa, na mavazi ya kifahari nk. Kumbuka hayo si matumizi sahihi ya faida uipatayo katika biashara yako.

Njia ya  nne; Ni kuwa mkarimu wakati wote  wa kufanya bishara yako, ukarimu ni sumaku ya kuvuta wateja, hakikisha una kuwa na wafanyakazi waliofundishwa ukarimu kwenye  bishara yako na matokeo yake ambayo ni biashara yako kustawi utayaona.

Njia  ya  tano; Jitenge wewe na bishara  yako, siku zote ione bishara yako kama mtu mwingine anayehitaji kuheshimiwa, jione kama  wewe ni mfanyakazi uliyepewa kazi ya  kuifanya bishara hiyo ili ikue, hiyo  itakusaidia kuwa na nidhamu juu ya bishara yako.

Njia ya sita; baini mbinu mpya zenye kuleta  tija katika bishara yako, muda wote jikite kwenye kufanya tafiti na kubaini njia mpya  zinazoweza kuongeza wateja katika bishara  yako. 

Mfano kuna mfanyabishara mmoja wa bucha ya kuuza nyama aliamua kutoa ofa ya kila anayenunua nyama kwake anapata nyanya mbili  bure, mbinu hiyo kiukweli ilivuta wateja wengi kwake na hivyo kustawisha biashara yake.

Njia ya saba; Tafuta uzalishaji nafuu wa bishara yako, kumbuka hakuna mteja anayependa kuumia katika upande wa bei ya huduma au  bidhaa fulani,ukiwa na uzalishaji wa chini wa bidhaa zako itakusaidia kuweka bei kuwa ya kawaida na wateja wengi kuimudu.

Bila shaka wewe msomaji umefuatilia kwa  makini Makala hii na naamini kila jambo linawezekana kama litafunguliwa njia, na njia hiyo ni wazo litakaloiingia kwenye utekelezaji na uthubutu.

Neno la faraja ni kwamba "kuzaliwa maskini  sio makosa bali kufa maskini ni makosa".

No comments:

Powered by Blogger.