LIVE STREAM ADS

Header Ads

SIKILIZA WALICHOKISEMA MADAM RITA, MASTER J NA SALAMA KUHUSU SHINDANO LA BSS 2015.

Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmack Production inayoandaa shindano la Bongo Star Search Rita Paulsen a.k.a Madam Rita, katika Judge Master J na Kulia ni Jugde Salama Jabir.
Na:George GB Pazzo
Majaji wa Shindano la Kusaka Vipaji hapa nchini la Bongo Star Search wamesema kuwa maboresho makubwa yamefanyika katika kuliboresha shindano hilo hivyo mwaka huu litakuwa tofauti ikilinganishwa na miaka iliyopita.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Benchmack Production inayoandaa shindano hilo Rita Paulsen maarufu kwa jina la Madam Rita ambae pia ni Jaji Mkuu pamoja na Majaji wasaidizi Master na Salama Jabiri walibainisha hayo wikendi iliyopita Jijini Mwanza wakati wa Usaili wa kuwasaka wawakilishi watakaoiwakilisha Kanda ya Mwanza katika Shindano hilo litakalofanyika Jijini Dar es salaam.

“Mashindano ya Mwaka huu yanafanyika mwaka wa nane hivyo uzoefu wa miaka minane ni Mkubwa sana na kama unavyoona tumeanzia huku (Mwanza) halafu tutaenda Arusha, Mbeya na Dar es salaam…aaaah changamoto zipo kila siku maana kitu chochote kizuri hakikosi changamoto na changamoto zipo nyingi lakini tunazimudu”. Alisema Madam Rita ambae alibainisha kuwa BSS 2015 itaanza kuruka hewani kuanzia Julai 19 mwaka huu kupitia Star Tv na Clouds Tv.

“Kwa ufupi BSS tunasaka Vipaji na inshu mhimu ambayo tumeboresha mwaka huu ni malalamiko mengi ambayo tumekuwa tukiyasikia kwamba washindi inakuwaje mbona hawasikiki kwenye soko la muziki baada ya kushinda BSS…Ni inshu ambayo ilikuwa siyo kosa letu maana sie tulikuwa tukijua tukimpa mtu hiyo Milioni Hamsini ataenda kuwekeza kwenye Muziki kumbe walikuwa wanafanya vitu kinyume…Kuna warembo, gari, wapambe na pamba vilikuwa vinawachanganya hivyo mwaka huu tumebadilisha mfumo na tumesema washindi watakaoingia tano bora watasimamiwa na Tip Top Connection ili ile hela tuiwekeze kidogo kwenye muziki na tupunguze hizi lawama lawama”. Alisema Master J.

“Haya ni mashindano na sidhani kama kuna haja ya Kumwambia mtu kitu ambacho siyo sahihi, kama anakuja na hajui kuimba inabidi aambiwe kuwa hajui kuimba na kama anajua kuimba inabidi aambiwe kuwa anajua kuimba…Master J ni Producer Mkubwa na ndiyo maana Rita amemchagua kuwa hapa na mimi namshukuru masikio yangu ni mazuri hivyo kama ni kutenda haki tunajitahidi kila siku kutenda haki na kumwambia mtu kile anachostahili ili kama hawezi asipoteze muda wake”. Alisema Salama Jabir.

Bonyeza HAPA Kuona Picha za Usaili wa BSS 2015 Mwanza.
                        BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA

No comments:

Powered by Blogger.