MKURUGENZI WA MABASI YA J4 ATIWA MBARONI JIJINI MWANZA KWA TUHUMA ZA MAUAJI.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo akitoa taarifa kwa wanahabari hii leo ofisini kwake baada ya tukio la mauaji ya watu wawili Jijini Mwanza lililotolea usiku wa kuamkia leo majira ya saa nne usiku eneo la Buzuruga ambapo anaetuhumiwa kutekeleza mauaji hayo ni Mkurugenzi wa Mabasi ya J4 yanayofanya safari zake katika Mikoa ya Mwanza na Mara.
Na:Binagi Media Group
Jeshi la Polisi Mkoani
Mwanza linamshikilia Mkurugenzi wa Kampuni ya Mabasi ya J4 Juma Mahende (45) Mkazi
wa Nyakato Sokoni Jijini Mwanza, kwa tuhuma za mauaji ya kuwapiga risasi
Watu wawili.
Akizungumza
jana ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishina Msaidizi wa
Polisi Charles Mkumbo alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi Majira ya Saa nne
Usiku katika eneo la Stand ya Buzuruga Jijini Mwanza.
Alisema
kuwa mauaji hayo yalitokea baada ya kuibuka mzozo baina yao ambapo mtuhumiwa huyo
ambaye hatimae alitoa bastora yake na kuwafyatulia risasi na hivyo kuwauwa papo
hapo watu hao ambao ni Ally Mohamed (35) Mkazi wa Igoma na Cloud Steven Mwenye (39)
Mkazi wa Nyasaka.
“Wakati
Mkurugenzi wa magari ya J4 yanayofanya safari zake katika Mikoa ya Mwanza na
Mara anafunga ofisi yake majira yaa saa nne usiku, walitokea vijana wawili
ambao walianza kuzozana nae kabla ya Mkurugenzi huyo kutoa bastora na
kuwafyatulia risasi za kifuani watu hao hao na kuwaua”.
Kamishina
Msaidizi Mkumbo aliitaja Silaha iliyotumika katika mauaji hayo kuwa ni bastola
aina Browning yenye nambari 00092890 ambapo Polisi wanaendelea na uchunguzi wake
ili kubaini chanzo cha mauaji hayo kabla ya kumfikisha kizimbani mtuhumiwa huo
ili kujibu shitaka linalomkabiri.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo
Waandishi wa Habari
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo akitoa taarifa kwa wanahabari hii leo ofisini kwake baada ya tukio la mauaji ya watu wawili Jijini Mwanza lililotolea usiku wa kuamkia leo majira ya saa nne usiku eneo la Buzuruga ambapo anaetuhumiwa kutekeleza mauaji hayo ni Mkurugenzi wa Mabasi ya J4 yanayofanya safari zake katika Mikoa ya Mwanza na Mara.
No comments: