LIVE STREAM ADS

Header Ads

MKUU WA WILAYA YA MAGU ABAINISHA FURSA KUBWA YA UWEKEZAJI ILIYOPO WILAYANI HUMO.

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe.Karen Yusun
 Na:George GB Pazzo
Wawekezaji kutoka Sekta mbalimbali nchini wametakiwa kuchangamkia na kutumia fursa ya upatikanaji wa ardhi iliyopo katika Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza,  kwa ajili ya kuimarisha zaidi uwekezaji wao.

Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Wilaya ya Magu Karen Yusun wakati akizungumzia fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani humo na namna zinavyoinufaisha Wilaya hiyo.

Alisema hadi sasa makampuni mbalimbali yamejitokeza na kupokelewa vyema kwa ajili ya kuwekeza katika Wilaya hiyo, huku akiongeza kuwa mbali na makampuni hayo kunufaika kiuwekezaji, pia yamekuwa yakichangia katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo kushiriki katika ujenzi wa Maabara pamoja na kutoa ajira kwa wakazi wake.

“Makampuni haya yanayowekeza katika Wilaya yetu tumeyapokea vizuri na manufaa yake tumekuwa tukiyaona maana yamekuwa yakitoa ajira kwa watu wetu, pia yamekuwa yakichangia katika shughuli za maendeleo ya jamii ikiwemo ujenzi wa Maabara hivyo nitumie fursa hii kuyashukuru mashirika na makampuni yote ambayo tayari yamewekeza katika Wilaya yetu”. Alisema Yusun.

Akizungumzia uwekezaji wa Kampuni ya Mobisol inayojishughulisha na ukopeshaji na uuzaji wa Mitambo ya kuzalisha Umeme wa jua (Solar) ambayo imeweka Makao Makuu yake katika Ukanda wa Ziwa Wilayani Magu, Yunus alisema kuwa Kampuni hiyo imeingia wakati mwafaka Wilayani humo kwa kuwa maeneo mengi ya Wilaya hiyo bado hayana umeme wa Tanesco hivyo maeneo hayo yatafunaika na nishati ya umeme wa jua kwa ajili ya matumizi ya nyumbani pamoja na shughuli za kiujasiriamali.

“Kwa kweli Mobisol wamekuja wakati mwafaka maana kuna maeneo mengi bado hayajafikiwa na Umeme wa gridi ya Taifa hivyo wahakikishe kuwa wanayafikia maeneo hayo, lakini pia wananchi watumie vifaa vyao maana umeme ni maendeleo hivyo wanaweza kutumia vifaa hivyo kuzalisha umeme kwa ajili ya shughuli zao za kiujasiriamali”. Alitanabaisha Yunus na kuongeza kuwa;

“Wilaya ya Magu tumepima viwanja kwa ajili ya biashara na uwekezaji wa aina mbalimbali katika Maeneo ya Kuku Poa, katika Mji wa Kahangara na Kisesa hivyo wawekezaji wawe tayari kuvinunua viwanja hivyo kwa ajili ya uwekezaji, lakini pia tuko karibu na jiji la Mwanza ambalo sasa libebanana hivyo waje Magu na tutashirikiana nao vizuri”. Alidokeza Mhe.Yunus.

Bonyeza Play hapa chini Kusikiliza MAHOJIANO

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe.Karen Yusun

No comments:

Powered by Blogger.