LIVE STREAM ADS

Header Ads

KAIMU MKURUGENZI WA JIJI LA MWANZA NA MTATHIMINI WA JIJI HILO WAPANDISHWA KIZIMBANI.

"Wala Msiwe na Wasiwasi, nyie pigeni tu picha". Alikuwa akisema Mahinya (Wa kwanza) baada ya kutoka kusomewa mashtaka.
 Na:Binagi Media Group
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Jeremiah Tito Mahinya pamoja na Mtathimini wa Jijini hilo Ramadhan Seleman Kamese, wamepandishwa Kizimbani na kusomewa mashtaka ya tuhuma zinazowakabili za kutumia vibaya madaraka kwa kuidhinisha kiasi cha shilingi Milioni 161 kama vidia ya viwanja.

Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa TAKUKURU Mwema Mella, aliiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Kanda ya Mwanza kuwa mwaka 2012 watuhumiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kwa kuidhinisha kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kulipa fidia za viwanja katika eneo la Ilamba B, Nyamhongolo Jijini Mwanza bila idhini ya Mtathimini Mkuu wa Serikali.

Baada ya Kusomewa mashtaka hayo, watuhumiwa wote walikana tuhuma zinazowakabiri ambapo wameachiwa huru kwa kila mmoja kudhaminiwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja ametakiwa kutoa Shilingi Milioni 80 au mali isiyohamishika yenye thamani sawa na kiasi hicho cha fedha.

Kesi hiyo ambayo imekamilika upepelezi wake kwa upande wa Mashtaka, iliahirishwa na Hakimu Mfawidhi Mkoa wa Mwanza Wilbert Chuma hadi tarehe Saba Mwezi wa Tisa Mwaka huu itakapotajwa tena kwa mara ya pili.

No comments:

Powered by Blogger.