LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAJASIRIAMALI MKOANI MWANZA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO ILI KUKUZA MITAJI YAO.

Afisa Mikopo kutoka Sakosi ya Utoaji Mikopo kwa Wajasiriamali nchini ya Take and Back Financial Insitution Neema Joseph Jingu (Kushoto) akizungumza na GB Pazzo (Kulia) katika Ofisi za Sakosi hiyo zilizopo Jengo la CCM Mkoa wa Mwanza.
Na:George GB Pazzo
Wajasiriamali Mkoani Mwanza wameshauriwa kuchangamkia fursa za Mikopo zinazotolewa na taasisi mbalimbali za kifedha hapa nchini, kwa ajili ya kukuza mitaji ya biashara zao.

Ushauri huo ulitolewa jana na Afisa Mikopo kutoka Sakosi ya Utoaji Mikopo kwa Wajasiriamali nchini ya Take and Back Financial Insitution Neema Joseph Jingu wakati akizungumza na Radio Metro katika ofisi za Sakosi hiyo zilizopo Jengo la CCM Mkoani Mwanza.

Jingu alisema kuwa Wajasiriamali wanapaswa kuondokana na hofu ya kujitokeza kukopa katika taasisi hizo, kwa kuwa hatua hiyo itawasaidia kukuza biashara zao.

“Taasisi nyingi za fedha nchini ikiwemo Sakosi ya Take and Back Financial Insitution hutoa elimu ya Ujasiriamali kabla ya kutoa mikopo yake kwa wajasiriamali, jambo ambalo limesaidia wakopaji kumudu kurejesha mikopo yao kwa wakati”. Alibainisha Jingu.

Aidha alibainisha kuwa zaidi ya Wajasiriamali 400 wamenufaika na Sakosi hiyo Mkoani Mwanza, tangu kuanzishwa kwake mwezi Septemba Mwaka jana.

Hata hivyo baadhi ya Wajasiriamali waliozungumza na Radio Metro Jijini Mwanza, walisema kuwa bado taasisi za fedha zinazotoa mikopo kwa Wajasiriamali zina masharti magumu yanayosababisha kutonufaika na mikopo hiyo ambapo wameomba kupunguzwa kwa baadhi ya masharti hayo ambayo ni pamoja na riba kubwa sanjari na uhitaji wa hati ya nyumba ama kiwanja.

“Mimi kinachonichanganya kabisa katika hii mikopo ni kuanza kuulizwa hati ya nyumba au kiwanja wakati hauna. Hivyo mimi ningeomba hivyo vigezo wavipunguze”. Alisema kijana Benjamin Zacharia ambae ni mwenyeji wa Wilaya ya Misungwi anaefanya shughuli zake za ujasiriamali Jijini Mwanza.

Kwa pamoja Bi.Tatu Mussa pamoja na Kijana Rio Michael ambao ni Wajasiriamali Jijini Mwanza alisema riba kubwa, leseni, hati ya nyumba ama kiwanja pamoja na mirorongo mingine isiyo na tija inapaswa kuondolewa kwa wajasiriamali maana inazidi kuwadidimiza wajasiriamali.
Afisa Mikopo kutoka Sakosi ya Utoaji Mikopo kwa Wajasiriamali nchini ya Take and Back Financial Insitution Neema Joseph Jingu.
Afisa Mikopo kutoka Sakosi ya Utoaji Mikopo kwa Wajasiriamali nchini ya Take and Back Financial Insitution Neema Joseph Jingu.
Special Thanks to Radio Metro Fm.

No comments:

Powered by Blogger.