LIVE STREAM ADS

Header Ads

HII NDIYO KAULI YA MHE.ASHA-ROSE MIGIRO KWA WANAWAKE NCHINI.

Na:George GB Pazzo
Waziri wa Katiba na Sheria Asha Rose Migiro amewasihi Wanawake nchini Kushikamana kwa pamoja katika kutetea Maslahi ya Taifa hususani katika kuombea amani iliyopo katika kuelekea kwenye kipindi cha Uchaguzi Mkuu.

Migiro alitoa Kauli hiyo jana Jijini Mwanza alipokuwa akizungumza katika Kongamano la Wanawake na Maendeleo, lililoandaliwa na Asasi ya Nitetee Foundation kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa lengo la kuombea amani ya Taifa pamoja na Uchaguzi Mkuu.

Alisema kuwa ajenda ya wanawake nchini ni amani hivyo wanapaswa kushiriki ipasavyo katika kuienzi kwa vitendo amani hiyo ikiwa ni pamoja na kushiriki katika utatuzi wa matatizo ya kijamii ikiwemo kukemea ukatili katika jamii pamoja na kutetea maslahi ya wanawake.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mwajuma Nyiluka ametoa rai kwa wanawake kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu nchini unafanyika kwa amani  kwa kuwa wanayo nafasi hiyo kupitia maombi yao.


Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Asasi ya Nitetee Foundation ya Jijini Mwanza Flora Lauwo amewaomba wadau mbalimbali kushirikiana na asasi hiyo ili kufanikisha malengo yake ambayo ni kutoa elimu juu ya masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo ujasiriamali, ukatili wa kijinsia, Mauaji kwa watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu nchini.
TAZAMA HAPA PICHA ZA KONGAMANO HILO

No comments:

Powered by Blogger.