LIVE STREAM ADS

Header Ads

RAIS MAGUFULI APONGEZWA.

Judith Ferdinand, Mwanza
Mwenyekiti wa mtaa wa Nyamanoro Mashariki Manispaa yaMkoani Mwanza, Trasisius Kabuche ampongeza Rais Magufuli, kwa hatua aliyochukua ya  kuelekeza fedha za sherehe ya Muungano inayoadhimishwa kila mwaka  Apili 26,  kutumika katika ujenzi wa barabara   kuanzia Nera mpaka uwanja wa Ndege wa Mwanza.

Kabuche amesema, hatua aliyochukua  Dkt.Magufuli ni ya kizalendo, kwani anaonyesha alivyo na uchungu na maendeleo ya  nchi.

Aliongeza kuwa , ni jambo jema kwa maendeleo ya taifa kwani kumekuwa na matumizi  mabaya ya  fedha, zinazotumika  katika maadhimisho ya sherehehe mbalimbali huku wananchi wakikosa huduma muhimu za kijamii.

Pia alisema, wananchi wamekuwa na kilio cha muda mrefu juu ya kupata kiongozi ambaye yuko tayari kutetea maslahi ya  taifa na kuleta maendeleo kwa jitihada na juhudi binanfsi.

Hata hivyo alimuomba Dkt.Magufuli kutoishai katika sherehe za Muungano, ila  aangalie na suala la mbio za Mwenge ambao unagharimu fedha za wananchi ,  na badala yake fedha hizo hazielekeze katika sekta ya elimu,  afya na ajira kwa vijana.

Aidha  aliongeza  kwa kumuomba Dkt.Magufuli kusimamia suala la katiba kwa ustawi wa maendeleo ya taifa kwa vizazi vijavyo,   kwani hili  nchi iendelee kukua kiuchumi  inaitaji mfumo ambao kila kiongozi atatakiwa kufuata kutokana na  utawala  kubadilika badilika   huku kiongozi  kwa wakati huo kuongoza atakavyo.

Wakati huo huo aliwaomba,  wananchi na viongozi mbalimbali kumuuunga mkono rais,  kwa kila mtu kuwajibika ipasavyo katika nafasi yake kiutendaji, ili kuleta maendeleo ya taifa na kuacha kutegemea msaada kutoka kwa wafadhili wa  nje.

No comments:

Powered by Blogger.