WATU WATATU WANAOSADIKIWA KUWA MAJAMBAZI WAUWAWA MKOANI MBEYA.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Butusyo Mwambelo akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya (Hawapo pichani)katika kuzngumzia tukio la kuuwawa kwa majambazi watatu wakati wakijaribu kufanya uhalifu katika duka la kuuzia vinywaji mji mdogo wa Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Butusyo Mwambelo akionyesha silaha aina ya SMG yenye namba 1996 AFU 1120 na risasi 26 kwenye magazine ambayo ilikuwa ikitumika na majambazi hao katika tukio la kutaka kufanya uhalifu kwenye duka la vinywaji mali ya Hamisi mji mdogo wa Matundasi Wilayani Chunya Mkoani Mbeya April 27 mwaka huu.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Butusyo Mwambelo akionyesha silahaaina ya panga ambalo linadaiwa kutumiwa na majambazi hao .
Baadhi ya askari polisi wakifuatilia kwa makini mkutano wa kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa mbeya Butusyo Mwambelo wakati akizungumza na waandsihi wa habari kufuatia tukio la kuuwawa kwa majambazi watatu waliotaka kufanya uhalifu katika duka la vinywaji vya jumla linalomilikiwa na ndugu Hamisi Mkazi wa Matundasi Chunya Mkoani Mbeya .
Silaha mbalimbali zilizo kamatwa katika tukio la kuuwawa kwa majambazi wilayani Chnua mkoani mbeya April27 mwaka huu.
Na
EmanuelMadafa, (Jamiimoja blogu-Mbeya)
JESHI la Polisi mkoani Mbeya limewauwa watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni
majambazi wakati wa kurushiana rasasi.
Kaimu
kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Butusyo Mwambelo amesema tukio hilo limetokea
April 27 mwaka huu saa 2 usiku , huko katika kijiji cha Matundasi Wilayani
Chunya Mkoani Mbeya .
Amesema watu
watano wanaosadikiwa kuwa ni majambazi
wakiwa na bunduki moja ya aina ya SMG yenye namba 1996 AFU 1120 na risasi 26
kwenye magazine , walifika kijijini hapo
kwa lengo la kufanya uhalifu kwenye duka la jumla la kuuzia
vinywaji mali ya Ndugu Hamis Mkazi wa
eneo hilo la Matundasi Chunya.
Kamanda
Mwambelo , amesema watu hao ambao miili yao imehifadhi kwenye chumba cha
mochwari katika hospitali ya wilaya ya
Chunya , majina na makazi yao bado hayajajulikana.
Akifafanua,
amesema taarifa za siri kutoka kwa raia wema zilifikia jeshi la polisi na ndipo
askari polisi walipofika kwenye eneo la tukio.
“Baada ya
polisi kufika katika eneo la tukio watu
hao walistuka kuwa wanafuatilwa na askari polisi na hivyo kuanza kukimbia
kuelekea kijiji cha Matondo kwa kutumia
pikipiki yenye namba za usajili MC 761. AFS
aina ya Sanlag yenye rangi nyeusi”,amesema Mwambelo.
Amesema
walipoona Polisi wanawakaribia walianza
kurusha risasi hovyo hewani
ambapo jambazi mmoja alijeruhiwa baada ya kupigwa risasi mguuni na tumboni na
kufariki dunia ambapo majambazi wanne walifanikiwa kutoroka .
Amesema
kutokana na hali hiyo jeshi hilo la polisi lilianzisha msako usiku huo na kufanikiwa kuwaua majambazi wengine wawili ambao huku wengine wakitoroka ambapo msako
mkali unaendelea ili kuwakamata wahalifu hao.
Amesema katika
eneo la tukio, ilipatikana bunduki moja aina ya SMG yenye namba 1996 AFU 1120
ikiwa na risasi 27 kwenye magazine. Pia pikipiki iliyokuwa iantumiwa na majambazi
hayo, iliwezea kupatikana pamoja na panga.
Mwambelo alitoa wito kwamba wananchi waendelee na moyo
huo huo wa kuwafichua watu wanaowatilia shaka ili waweze kudhibitiwa mapema
kabla ya kufanya uhalifu sanjali na kufika katika hospital ya wilaya ya Chunya
kwa lengo la kufanya utambuzi wa miili ya majambazi hao kwani majina yao bado
hayajatambulika.
No comments: