UJUMBE MAALUMU KUELEKEA SIKU YA KIMATAIFA YA KUONGEZA UELEWA KUHUSU WATU WENYE UALIBINO.
Katika kuelekea katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
kuongeza Uelewa dhidi ya Watu wenye Ualbino (International Albinism Awareness
Day) yatakayofanyika tarehe 13/06/2016,
Mimi Suleiman Magoma, mtanzania mwenye Ualbino pamoja na
tovuti yangu yawww.albinismtanzania.co.tz tumeandaa video clip fupi(kama
inavyoonekana hapo juu) yenye kutoa
Elimu ya Albinism kwa jamii ya
Watanzania wenzetu ili wawe na uelewa wa kutosha na hatimae kuachana na dhana,fikra na mitazamo potofu
kuhusu sisi watu wenye Ualbino.
Ewe mtanzania mwenzangu naomba uniunge mkono kwa kusambaza
hii Video Clip pamoja na caption yake kwa ndugu jamaa,marafiki,vyombo vya
habari, ma group mbalimbali ya whatsapp
pamoja na mitandao mbalimbali ya kijamii
ili elimu hii iweze kuwafikia watu wengi na hatimae utakuwa umesaidia
sana kupunguza au kukomesha kabisa vitendo vya Ukatili,Unyanyapaa na Mauaji ya
Watu wenye Ualbino katika nchi yetu. Tushirikiane katika kuhakikisha Elimu ya
Albinism inawafikia watu kadri inavyowezekana.
Suleiman Magoma
+255 766 467960
Suleiman.magoma41@gmail.com
www.albinismtanzania.co.tz
No comments: