LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA WAITEMBELEA MANISPAA YA ILEMELA MKOANI MWANZA.

Ikiwa Una Habari, Tukio, Picha, Maoni au Tangazo, Wasiliana Na BMG Kwa Nambari za Simu 0757 432694 Au Email binagimediagroup@gmail.com

Katika kuhakikisha wananchi wa wilaya ya Ilemela wanapata maendeleo ya haraka na yenye tija kwa kwenda sambamba na kasi ya serikali ya awamu ya tano, Wilaya ya Ilemela imefanikiwa kupokea wawekezaji kutoka nchini Korea kwa lengo la kuwekeza wilayani humo hasa kwenye sekta ya viwanda na kilimo.

Hayo yamebainishwa wiki hii na ndugu Amos Zephania kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa Ilemela alipokuwa akizungumza na wageni hao kata ya Sangabuye walipokwenda kufanya upembuzi yakinifu juu ya maeneo sahihi na fursa za uwekezaji zinazopatikana wilayani humo.

".. Kupitia wawekezaji hawa wananchi watapata ajira, miundombinu itaimarika sanjari na kuboresha maisha yao kunakochochewa na upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kwa uwekezaji huu.." Alisisitiza.

Pamoja na hayo wawekezaji hao wameahidi kuimarisha mahusiano waliyoyaanzisha na kuwa na tija kwa pande zote mbili.
Aidha ugeni huu ni matunda ya ziara ya Mhe Mbunge wa jimbo la Ilemela Dkt. Angeline Mabula alipotembelea nchini Korea Kusini mapema June 2016 ikiwa ni jitihada za kufungua milango ya maendeleo ya Jimbo hilo.

"Ilemela ni yetu,tushirikiane kuijenga"
Imetolewa na 
Ofisi ya mbunge
Jimbo la ilemela-mwanza

No comments:

Powered by Blogger.