Mafunzo kwa wafanyakazi wa nyumbani, waajiri pamoja na watendaji Jijini Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Binagi Media Group
Utafiti
uliofanywa na Shirika la hutetea haki za watoto wafanyakazi wanyumbani WOTESAWA
Jijini Mwanza, unaonyesha kwamba watoto hao bado wanakumbana na aina mbalimbali
za ukatili ikiwemo utumikishwaji.
Utafiti huo
uliofanyika mwaka jana ulibaini kwamba asilimia 91.9 ya watoto wafanyakazi wa
nyumbani katika Kata nne za Jiji hilo hawana mikataba ama makubaliano baina ya
wazazi na waajiri wao, asilimia 5.4 wana mikataba huku asilimia 80 ikionyesha
wapo wanaofanya kazi bila malipo huku wanaolipwa mshahara chini ya shilingi
20,000 wakiwa ni asilimia 20.
Utafiti huo
ulifanyika katika Kata za Igogo ambapo watoto wafanyakazi wa nyumbani 43
walifikiwa, Mkuyuni 42, Nyamagana 32 pamoja na Butimba 37 na hivyo kufanya
idadi ya watoto wafanyakazi wa nyumbani waliofikiwa kuwa 154, wavula wakiwa ni
16 na wasichana 138.
Washiriki wa semina hiyo wakimsikiliza Mkurugenzi wa WOTESAWA, Angel Benedicto, hii leo.
Mkurugenzi wa WOTESAWA, Angel Benedicto akizungumza kwenye semina hiyo
Washiriki wa semina hiyo wakimsikiliza Mratibu wa Shirika la WOTESAWA
Mratibu wa Shirika la WOTESAWA, Elisha Daud akiwasilisha mada kwenye semina hiyo
Mratibu wa Shirika la WOTESAWA, Elisha Daud akiwasilisha mada kwenye semina hiyo
Mmoja wa washiriki wa semina hiyo akiandika maazimio
Washiriki wa semina hiyo
Diwani wa Kata ya Butimba, John Pambalu akitoa salamu za shukurani wakati wa tamati ya semina hiyo
Washiriki
Ukumbi wa pili, semina kwa watoto wafanyakazi wa nyumbani pamoja na waajiri wao
Semina kwa watoto wafanyakazi wa nyumbani pamoja na waajiri wao
Picha ya pamoja
Bonyeza HAPA uchaguzi wa viongozi wa watoto wafanyakazi wa nyumbani
No comments: