Wanafunzi waibukia kwenye mkutano wa mbunge wa Bukombe
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Mbunge wa jimbo la Bukombe mkoani Geita, Mhe.Doto Mashaka Biteko (CCM) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini ameendelea na ziara yake katika Kata mbalimbali jimboni humo ili kuwaeleza wananchi utekelezaji wa ahadi zake za maendeleo pamoja na serikali ya awamu ya tano.
Akiwa katika Kata ya Butinzya jana, wanafunzi wa shule ya sekondari katika Kata hiyo waliibuka kwenye mkutano wake wa hadhara na kumuuliza maswali kuhusu changamoto zinazoikabili shule yao na namna atakavyowasaidia kuzitatua.
Na George Binagi, Bukombe
No comments: