Serikali yatatua adha ya usafiri kwa Maafisa Elimu Mwanza
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
SOMA Mkuu wa Mkoa Mwanza akabidhi pikipiki kwa Maafisa Elimu
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Serikali
kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa pikipiki kwa Maafisa Elimu Kata mkoani
Mwanza ili kuwaondolea adha ya usafiri na kuongeza ufanisi na utendaji kazi
katika Kata zao.
Kwa upande
wa Jiji la Mwanza (Nyamagana), Maafisa Elimu katika Kata zote 18 wamekabidhiwa
pikipiki zao hii leo Septemba 10, 2018 na Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe. John
Mongella ambaye amewahimiza kuzitumia vyema ili kufikia malengo yaliyokusudiwa
ya kurahisisha utendaji kazi wao.
Kaimu Afisa
Elimu Jijini Mwanza Philipo Mukama amesema pikipiki hizo zina gharama ya
shilingi milioni 54 na kwamba zimetolewa kupitia program ya EQUIP na LANES.
Tazama BMG Online Tv hapa chini
SOMA Mkuu wa Mkoa Mwanza akabidhi pikipiki kwa Maafisa Elimu
No comments: