LIVE STREAM ADS

Header Ads

Wanahabari Mwanza watakiwa kuandika habari na makala kuhusu malezi bora ya watoto

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Matangazo.

Judith Ferdinand, Mwanza
Wanahabari mkoani Mwanza wametakiwa kuandika habari za kuelimisha jamii kuhusu masuala ya watoto hususani malezi bora.

Hii ni baada ya kuonekana kuwa changamoto kubwa inayowakabili watoto na kupelekea kukosa haki zao katika Mkoa wa Mwanza ni kutokana na  wazazi kukosa elimu na kutokuwa na uelewa kuhusu malezi bora (chanya).

Wito huo umetolewa na Mratibu  wa Utetezi na Ushawishi wa Haki za Watoto wa Shirika la SOS Children  Village's Tanzania,  Mpelly Kalonge katika semina ya wadau kuhusu majadiliano  ya  utekelezaji wa sera, mipango na mikakati inayohusu mtoto ili kuwalinda watoto dhidi ya ukatili iliyowakutanisha jumla ya wadau 28 kutoka Kata sita ambazo mradi wa kuimarisha familia unafanya kazi ikiwemo Igogo, Mkuyuni, Pamba, Mhandu, Mahina na Bugongwa.

Kalonge alisema, kupitia semina hiyo wadau walisema changamoto kubwa inayowakabili watoto ni ukosefu wa elimu na malezi bora kutoka kwa wazazi hivyo ushawishi na uteteze wa haki za watoto ni jambo linalohitajika, hivyo ili jamii iweze kupata elimu ya malezi vyombo vya habari vinatakiwa kuandika na kuhabarisha habari zinazohusu watoto ikiwemo malezo chanya yanayotakiwa kwani kupitia wao ni rahisi kufikia watu wengi na kwa wakati mmoja.

No comments:

Powered by Blogger.