Waziri Biteko akutana na Mkurugenzi Mkuu NEMC
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na Nuru Ikupa, Dodoma
Waziri wa
Madini, Doto Biteko amekutana na Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi
na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka Mafwenga, ofisini kwake
jijini Dodoma.
Biteko
ameshukuru Dkt. Mafwenga kwa kuonesha nia ya kuwasaidia wachimbaji wadogo
kupata cheti cha mazingira baada ya kubainisha njia bora za kuwawezesha
wachimbaji wadogo kupata uelewa juu ya uhifadhi wa mazingira.
Akizungumza
katika kikao hicho kilichofanyika Januari jana, Dkt. Mafwenga alisema
kutokana na mwamko mkubwa iliyonayo Serikali wa kuwasaidia wachimbaji wadogo
kukua na kufanikiwa katika sekta ya uchimbaji mdogo wa madini, Nemc itajikita
katika kuhakikisha inashirikiana na wizara katika kuhamasisha na kuelimisha
wachimbaji wadogo juu ya umuhimu wa uhifadhi wa mazingira.
Aidha alibainisha kuwa, kutokana na vigezo vya awali ambavyo viliwafanya wachimbaji
wadogo kutokupewa cheti cha mazingira zitaboreshwa na kuwawezesha kupata cheti
hicho.
Alisema wachimbaji wadogo watapaswa kusajili miradi yao katika Ofisi za Kanda za Baraza
la Hifadi la Mazingira ambao watakagua
miradi hiyo na baada ya kujiridhisha watawapatia vyeti hivyo.
Waziri wa
Madini, Doto Biteko (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu
wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dr. Samuel
Gwamaka Mafwenga (kulia) pamoja na Meneja wa Kanda ya Kati, Arnold Mapinduzi (kushoto) baada ya kumaliza mazungumzo mafupi ya namna ya kuwawezesha wachimbaji
wadogo kuhifadhi mazingira.
No comments: