LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANZA: NEC kuboreshaji daftari la wapiga kura "si wote wataandikishwa"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeendelea na zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika mikoa mbalimbali nchini ambapo kwa Mkoa Mwanza zoezi hilo linatarajiwa kuanza Jumanne Agosti 13, 2019 hadi Jumatatu Agosti 19, 2019 katika vituo zaidi ya 2000.

Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mbarouk Salim Mbarouk ameyasema hayo leo Agosti 02, 2019 kwenye mkutano baina ya Tume hiyo na wadau wa uchaguzi mkoani Mwanza, uliowahusisha viongozi wa vyama vya siasa, dini, asasi za kiraia, makundi ya watu wenye ulemavu, vijana, wanawake na wanahabari.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.