Bashe aombwa kusaidia uendelezaji Kituo cha Utafiti wa Kilimo wilayani Chato
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Naibu Waziri
wa Kilimo, Hussein Bashe kupitia wizara hiyo ameombwa kusaidia uendelezaji wa
Kituo cha Utafiti wa Kilimo Bwanga kilichopo Wilaya Chato mkoani Geita ili kisaidie
kuongeza tija kwa wakulima.
Mkuu wa
Wilaya Chato, Mtemi Msafiri alitoa ombi hilo jana Agosti 03, 2019 wakati akitoa
salamu za Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel kwenye ufunguzi rasmi wa
maonesho ya Nane Nane Kanda ya Ziwa Magharibi yanayofanyika kwenye uwanja wa
Nyamhongolo jijini Mwanza.
Katika
ufunguzi huo, salamu za Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella ziliwasilishwa na
Mkuu wa Wilaya Sengerema, Mwl. Emmanuel Kipole aliyebainisha kwamba uzalishaji
umeendelea kuongezeka kwenye mazao ya kilimo hatua ambayo itakasaidia kufikiwa
kwa uchumi wa viwanda.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: