LIVE STREAM ADS

Header Ads

Machinga jijini Mwanza wawakingia kifua wateule wa Rais "tusichonganishwe"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
 Muungano wa Machinga Mkoa Mwanza umesema hakuna mgogoro wowote baina yao na wateule wa Rais kufuatia agizo la kuwaondoa baadhi ya wafanyabiashara wakubwa waliokuwa katika eneo la Pamba kwa kigezo kwamba nao ni machinga.

Wafanyabishara hao walijenga makontena katika eneo hilo baada ya kupisha mradi wa ujenzi wa soko kuu jijini Mwanza kwa kigezo kwamba nao ni machinga hatua ambao ilipingwa vikali na viongozi wa machinga wakisema hizo ni mbinu za ukwepaji kodi na kwamba machinga waliopisha mradi huo tayari wamehamia eneo la Mitimirefu.
#BMGHabari
 Mmoja wa machinga jijini Mwanza akizungumza na BMG.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.