LIVE STREAM ADS

Header Ads

Maonesho ya taasisi za fedha Mwanza "wakulima wahimizwa kujiunga na TAHA"

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amewahimiza wakulima wa mbogamboga na matunda kujiunga na kujiunga na taasisi ya TAHA (Tanzania Horticultural Association) ili kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana kupitia taasisi hiyo ikiwemo dhamana za mitaji na masoko.

Mongella ametoa rai hiyo wakati akifungua Maonesho ya Taasisi za Fedha kuhusu fursa za upatikanaji wa mitaji kwenye sekta ya Kilimo yanayofanyika kwa siku mbili kuanzia Novemba 15, 2019 katika eneo la Rock City Mall.

Maonesho hayo yameandaliwa na taasisi ya TAHA yakiwa na kaulimbiu isemayo “upatikanaji wa mitaji ya uhakika kwa ukuaji wa kilimo biashara kuelekea uchumi wa viwanda” inayolenga kuchochea upatikanaji wa mitaji kwa wakulima kupitia taasisi za kifedha.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye ufunguzi wa maonesho hayo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya TAHA, Peter Gongoseke akitoa salamu zake kwenye ufunguzi wa maonesho hayo.
 Mkurugenzi Mtendaji TAHA, Jacqueline Mkindi akitoa ufafanuzi kuhusiana na maonesho hayo.
 Afisa Mahusiano Kitengo cha Biashara kutoka StanBank, Samson Maduka akitoa salamu za benki hiyo ambayo ni mdhamini wa maonesho hayo.
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akipata maelezo baada ya kutembelea banda la TAHA kwenye maonesho hayo.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akikagua mabanda mbalimbali.
Tazama BMG TV ONLINE hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.