DC Magu ahimiza wananchi kuendelea kujifukiza
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa
Wilaya Magu mkoani Mwanza, Dkt. Philmon Sengati amewahimiza wananchi kuendelea
kuzingatia tahadhari za kujikinga na maambukizi dhidi ya virusi vya Corona
(Covid- 19) ikiwemo kutumia njia za asili za kujifukiza kama ilivyoshauriwa na
Rais Dkt. John Magufuli.
Dkt. Sengati
ameyasema hayo Jumatano Aprili 29, 2020 wakati akipokea mashine tano za kupima
joto la mwili pamoja na vitakasa mikono lita 10 zilizoolewa na Shirika la
KIVULINI ili kuunga mkono jitihada za Serikali katika kupambana na Corona.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Shirika la KIVULINI limekabidhi vifaa vya kusaidia mapambano dhidi ya Corona katika Wilaya Magu vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.8 (Tsh. Milioni 1,840,000).
Wafanyabiashara wa soko kuu mjini Magu wakipima joto la mwili baada ya kupokea kifaa cha huduma hiyo kutoka Shirika la KIVULINI.
Tazama BMG TV hapa chini
PIA SOMA>>> Habari mbalimbali kuhusiana na Corona
No comments: