LIVE STREAM ADS

Header Ads

RC Mongella azindua zoezi la kutoa elimu ya kujikinga na Corona

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amezindua rasmi zoezi la kutoa elimu na kusambaza vipeperushi vyenye ujumbe wa namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (Covid- 19) katika maeneo mbalimbali ya umma ikiwemo masoko na vituo vya usafiri.

Zoezi hilo linalotekelezwa na Chama cha Msalaba Mwekundu Tanzania (RED CROSS) kwa kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. Uzinduzi huo umefanyika Aprili 01, 2020 ukiambatana na utoaji elimu ya kujikinga na Corona kwa watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa Mwanza.

Katika kuhakikisha afua za kupambana na Corona zinatekelezwa, Mongella amekagua utayari wa kupambana na maambukizi ya ugonjwa huo katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu ikiwemo kivuko cha Kigongo-Busisi, stendi ya mabasi Nyabulogoya, soko la Mirongo na Mbugani ambapo amewahimiza wananchi kuzingatia tahadhari zinazotolewa na Serikali ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza na watumishi wa sekretarieti ya Mkoa Mwanza kabla ya kuzindua zoezi la usambazaji vipeperushi vyenye ujumbe wa kujikinga na Corona.
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akipokea kipeperushi kutoka kwa Mratibu wa RED CROSS Mkoa Mwanza, Salome Tuppa (kushoto).
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akipokea bango lenye ujumbe wa namna ya kujikinga na Corona kutoka kwa Mratibu wa RED CROSS Mkoa Mwanza, Salome Tuppa ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa zoezi la kusambaza mabango na vipeperushi hivyo kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akigawa kipeperushi chenye ujumbe wa namna ya kujikinga na Corona. 
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akigawa kipeperushi chenye ujumbe wa namna ya kujikinga na Corona kwa watumishi wa sekretarieti ya Mkoa Mwanza. 
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kulia) akigawa kipeperushi chenye ujumbe wa namna ya kujikinga na Corona.  
Tazama BMG TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.