Musukuma azua balaa “apewa onyo kali”
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mwenyekiti
wa Kamati inayosimamia zoezi la upuliziaji wa dawa ya kuangamiza virusi vya Corona
kwenye vyombo vya usafiri mkoani Mwanza, Yusuph Lupilya amemuonya mbunge wa
Geita Joseph Kasheku “Musukuma” ambaye pia ni mdau wa usafirishaji kuacha mara
moja kupotosha umma juu ya zoezi hilo alilodai linatekelezwa bila kufuata
utaratibu.
Lupilya
ametoa onyo hilo Jumamosi Aprili 11, 2020 wakati akiendelea kusimamia zoezi la
upuliziaji dawa hiyo kwenye vyombo vya usafiri katika vituo mbalimbali jijini
Mwanza ikiwa ni siku moja tu baada ya Musukuma kugomea zoezi hilo.
#BMGHabari
Timu ya upuliziaji dawa ya kuangamiza virusi vya Corona katika vyombo vya usafiri mkoani Mwanza ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa afua za kupambana na maambukizi ya virusi hivyo.
Zoezi la upuliziaji dawa ya kuangamiza maambukizi ya virusi vya Corona katika vyombo vya usafiri mkoani Mwanza ikiwa ni tahadhari ya kupambana na maambukizi ya virusi hivyo.
Tazama BMG TV hapa chini
No comments: