LIVE STREAM ADS

Header Ads

MONGELLA apokea shehena ya mabomba ya maji “Serikali haisimami”

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amepokea shehena ya vifaa mbalimbali ikiwemo mabomba kwa ajili ya kutekeleza miradi 22 ya maji yenye thamani ya shilingi bilioni nane katika maeneo ya vijijini.

Mongella amepokea shehena hiyo Septemba 22, 2020 na kuikabidhi kwa wakala wa usambazaji maji vijijini (RUWASA) kwa ajili ya kuanza kazi ya kutandaza mtandao wa maji katika Wilaya za Misungwi, Magu, Kwimba, Sengerema na Ukerewe.

“Kwenye Uchaguzi Serikali haisimami ili kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma, kazi kubwa sasa ni kusimamia miradi hii ili ikamilike na ikiwezekana kabla ya wakati kwani Serikali imesimamia vifaa vimefika” alisisitiza Mongella.

Tazama BMG ONLINE TV hapa chini

SOMA>>> Mongella akiwa kazini

No comments:

Powered by Blogger.