LIVE STREAM ADS

Header Ads

Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa maji Bugayambelele Shinyanga

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama ripotabmg@gmail.com
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim (kushoto) akimtwisha ndoo kichwani Fortunatha Allan wakati akizindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim (kushoto) akimtwisha ndoo kichwani mkazi wa Bugayambelele wakati akizindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023.


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdallah Shaib Kaim amezindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) wenye thamani ya Shilingi 279,465,134.40.

Akizungumza leo Alhamisi Julai 28,2023 baada ya kukagua mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim ameipongeza SHUWASA kwa kutekeleza mradi wa maji kwa kiwango bora na thamani ya fedha imeonekana.

“Tumekagua mradi na nyaraka kwa kina, kazi nzuri imefanyika hivyo Mwenge wa Uhuru unazindua Mradi huu. Naipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa inayofanya katika utekelezaji wa miradi maji ili kumtua mama ndoo kichwani”,amesema Kaim.
Akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel amesema mradi huo unatarajiwa kunufaisha wakazi 10,165 kwa kuwawezesha kupata huduma ya majisafi na salama kutoka katika mtandao huo na kuwafanya waondokane na adha ya kufuata maji mbali kama ilivyokuwa hapo awali kwa kuongeza eneo la huduma na kuweka mabomba makubwa ya usambazaji wa maji.

Amesema kwa sasa utekelezaji wa mradi umefikia asilimia 100 ya utekelezaji wake na huduma inaendelewa kutolewa kwa wananchi.

Amesema Mradi huo wa Maji katika Kijiji cha Bugayambelele – Manispaa ya Shinyanga ulisanifiwa na Wakala wa Maji Vijijini (RUWASA) Shinyanga kwa kuongeza mtandao wa maji kilometa 8.041 ambapo awali RUWASA ilijenga kilometa 1.5 na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) ilijenga kilometa 6.459.

“Uongozi wa Mkoa wa Shinyanga unaendelea kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutekeleza Miradi ya Maji na kupunguza adha kwa wananchi ya kutopata majisafi, salama na yenye kutosheleza”,amesema.

Nao baadhi ya wananchi akiwemo Mzee John Maganga Midelo (103) na Fortunatha Allan Malongo wameishukuru serikali kuwa kuwapelekea mradi wa maji kwani walikosa huduma hiyo kwa muda mrefu na sasa wameanza kupata huduma ya maji safi na salama.

“Tunamshukuru sana Mhe. Rais Samia kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya kuleta maendeleo. Kiongozi wa mbio za Mwenge nakuomba upeleke salamu kwa Mhe. Rais Samia kwamba sisi tunampenda sana, aendelee kuchapa kazi ili kuwaletea maendeleo Watanzania”,amesema Mzee Midelo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim akizindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023. 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim (katikati) akizindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini , Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim (kushoto) akimtwisha ndoo kichwani Fortunatha Allan wakati akizindua rasmi Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim na viongozi mbalimbali wakipiga makofi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim na viongozi mbalimbali wakipiga makofi wakati wa uzinduzi rasmi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim akizungumza katika Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim akizungumza katika Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel akisoma taarifa ya ujenzi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel akielezea kuhusu ujenzi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Mkazi w Bugayambelele Fortunatha Allan akiishukuru Serikali kujenga Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel akisoma taarifa ya ujenzi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Julai 28,2023
Viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa wakikagua nyaraka za ujenzi wa Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Muonekano sehemu ya mradi wa maji
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi akizungumza katika Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Mzee John Maganga Midelo akiishukuru serikali kupeleka mradi wa maji katika Kijiji cha Bugayambelele. Kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, kulia ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim
Mzee John Maganga Midelo akishika Mwenge wa Uhuru. Kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, kulia ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim
Mzee John Maganga Midelo akishika Mwenge wa Uhuru
Wafanyakazi wa SHUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Wajumbe wa bodi ya SHUWASA na viongozi wa RUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Wafanyakazi wa SHUWASA na RUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel akisalimiana na Mzee John Maganga Midelo
Wafanyakazi wa SHUWASA wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye Mradi wa Maji Safi na Salama kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga
Meneja wa RUWASA Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Julieth Payovela na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel (kulia) wakipiga picha ya kumbukumbu
Meneja wa RUWASA Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Julieth Payovela na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa SHUWASA CPA Sarah Emmanuel (kulia) wakipiga picha ya kumbukumbu.

No comments:

Powered by Blogger.