LIVE STREAM ADS

Header Ads

Serikali yaombwa kusaidia gharama za machapisho ya kufundishia vyuoni

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Waziri Mkuu, Sakina Mwinyimkuu ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua kongamano la kisayansi ambalo limeandaliwa na Shirikisho la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL) kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi


Na Dotto Mwaibale, Singida
Shirika la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL) limeiomba Serikali kupitia ofisi ya Waziri Mkuu kusaidia kununua machapisho ya kielekitroniki yanayotumika kufundishia vyuoni kwa kuwa yanauzwa bei ghali ambayo shirikisho hilo haliwezi kumudu kuyanunua.

Mwenyekiti wa Shirikisho hilo , Dkt. Sydney Msonde alitoa ombi hilo Novemba 09, 2023 wakati wa ufunguzi wa kongamano la kisayansi ambalo limewakutanisha wanataaluma mbalimbali katika ngazi ya wakutubi, walimu wafundishaji kutoka vyuo vikuu Tanzania Bara na Visiwani, watafiti pamoja na watu wanaoshughulika na masuala ya teknolojia (IT)

Amesema pamoja na kwamba lengo la COTUL ni kuhakikisha kwamba machapisho ya kielekitroniki yanapatikana kwa walimu na wanafunzi ili waweze kufanya shughuli zao za msingi za kujifunza, kufundisha na kufanya utafiti hapa nchini lakini kununua machapisho hayo imekuwa changamoto kutokana na kuuzwa bei ghali.

Dkt. Msonde ametoa mfano uchapishaji wa kanzi data inayoitwa 'Sience Direct' ambayo inauzwa dola za Marekani 250,000 hivyo sio rahisi kwa taasisi moja za hapa nchini kuweza kumudu kununua chapisho kama hilo.

“COTUL kazi yetu kubwa ni kuhamasisha na kuzileta pamoja taasisi zote za umma na za watu binafsi ili ziweze kuchangia kwa sehemu rasilimali fedha zitakazo wezesha kununua machapisho hayo ya msingi katika kukidhi haja ya kufanya ufundishaji na utafiti nchini” amesema Dkt. Msonde.

Dkt. Msonde amesema uhaulishaji na upatikanaji wa machapisho hayo unaweza usiwe na tija kama walimu na wanafunzi watakao kuwa wanayatumia hawatajengewa uwezo bora wa kuyatumia jambo ambalo ndilo la msingi.

Amesema lengo la kongamano hilo ni kujadili mustakabari wa fani ya ukutubi na namna gani walimu katika taasisi za umma na watu binafsi wanaweza kutumia machapisho ya kielekitroniki katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi Tanzania.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Waziri Mkuu, Sakina Mwinyimkuu amepongeza COTUL kwa kupiga hatua kubwa katika kipindi cha miaka 15 tangu shirikisho hilo lilipoanzishwa mwaka 2008.

Amesema shirikisho hilo limekuwa msaada mkubwa kwa serikali kwa kuisaidia kupata taarifa na maarifa mbalimbali ambayo kwa njia ya kawaida ingekuwa ni gharama kubwa kuyapata.

"Uwepo wa COTUL ni fursa hata kwa sisi tunaohusika na kufanya tathmini mbalimbali zikiwemo za utafiti hakika ni jukwaa muhimu sana" amesema Mwinyimkuu.

Mwinyimkuu amesema Serikali itaendelea kuunga mkono kazi zinayofanywa na COTUL na kuliomba shirikisho hilo kukutana na wadau wa elimu ndani ya Serikali ili waone namna ya kushirikiana nao na kuwa kazi zao zinazihitaji na hazikwepeki hasa katika kipindi hiki ambacho dunia inahitaji teknolojia kwa ajili kukuza uchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB), Dkt. Mboni Ruzegea amesema Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan inafanya maboresho makubwa ya maktaba kutoka katika mfumo wa kuhifadhi vitabu na machapisho mengine kwa njia ya kizamani ya karatasi na kwenda kwenye mfumo wa kidijitali.

Mmoja wa wafadhili wa kongamano hilo Mkurugenzi wa Kampuni ya Totoo Ltd yenye makao yake makuu mkoani Kilimanjaro, Dkt. Elvis Silayo amesema changamoto kubwa inayowafanya watu wengi washindwe kuitumia maktaba kwanza wanakuwa hawajui taarifa ambazo wanaweza kuzipata na imekuwa ikichukuliwa kama sehemu ya taaluma na inatakiwa kuwa mashuleni.

Amesema watu wengi hawapendi kusoma mambo ya taaluma lakini maktaba kuna taarifa nyingi ambazo wanaweza kuzipata na kuwasaidia kupata maarifa yanayoweza kuwasaidia katika maisha yao ya kila siku.

Amesema maktaba za sasa zinavitabu vilivyochapishwa kwenye miaka ya 70 na 80 hivyo taarifa zake haziwezi kuwa na msaada kwa mtu anayehitaji kufanya chochote kwa kipindi hiki na kueleza kuwa maktaba za sasa zinapaswa kwenda mbele zaidi kwa kuwa na taarifa ambazo zinakwenda na wakati.

Silayo amesema ile dhana iliyozoeleka kuwa maktaba zipo kwa ajili ya kumuandaa mwanafunzi afaulu mtihani sasa iachwe badala yake zitumike kuwaandaa kimaisha.

Naye Mhadhiri wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dkt. Valeria Kyumana amesema mafunzo hayo yamewajenga kwasababu hivi sasa teknolojia inakuwa na maktaba na huduma wanazotoa haziwezi kuendelea kwa kutumia mfumo wa zamani waliokuwa wakiutoa.

“Lazima tuangalie teknolojia inavyokwenda tukue nayo na kama sisi wakutubi tuweze kuichukua na kuitoa kwa wateja wetu tunaowahudumia ambao ni wanafunzi na watu wengine” amesema Kyumana.

Baadhi ya wadhamini wa kongamano hilo ni Totoo Company Ltd, Ebsco, Elsevier, Jove, Buku,Eclat, Bookstore, emerad insight, TCC na LexisNexis.Mkurugenzi wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB), Dkt. Mboni Ruzegea akizungumza kwenye kongamano hilo.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL), Dkt. Sydney Msonde akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.
Katibu Mkuu Chama cha Wakutubi Tanzania (TLA), Dkt Rhodes Mwageni akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Maktaba za Vyuo Vikuu na Taasisi zinazofanya Utafiti Tanzania (COTUL), Dkt. Vincent Msonge akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Totoo Ltd yenye makao yake makuu mkoani Kilimanjaro, Dk. Elvis Silayo akizungumza kwenye kongamano hilo.
Keki ya kutimiza miaka 15 tangu kuzaliwa kwa COTUL mwaka 2008 ikikatwa
Makamu Mwenyekiti COTUL, Profesa Kelefa Mwamtimwa, akitoa neno la shukurani kwa mgeni rasmi na wadau wengine wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo.
Wakutubi wakiwa kwenye kongamano hilo.
Viongozi wakiwa meza kuu.
Kongamano likiendelea.
Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Wakutubi wakiwa kwenye kongamano hilo.
Viongozi meza kuu wakishiriki kuimba wimbo wa Taifa kabla ya ufunguzi wa kongamano hilo.
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Wakutubi wakionesha moja ya ishara ya mshikamano.
Viongozi wa COTUL wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi, Mkurugenzi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Waziri Mkuu, Sakina Mwinyimkuu (katikati waliokaa) baada ya kufungua kongamano hilo Novemba 09, 2023.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi.
Picha ya pamoja.
Picha ya pamaja ba mgeni rasmi
Picha ya pamoja.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa kongamano hilo.
Picha ya pamoja mgeni rasmi na washiriki wa kongamano hilo.

No comments:

Powered by Blogger.