LIVE STREAM ADS

Header Ads

BINTI WA KAZI ZA NDANI ANUSURIKA KUBAKWA NA BOSI WAKE (BABA MWENYE NYUMBA) JIJINI MWANZA.

Binti alienusurika Kubakwa.

Binti Mmoja mwenye Umri wa Miaka 15 (Jina tumelihifadhi) Mwenyeji wa Mkoani Tabora ambae alikuwa akifanya kazi za ndani Jijini Mwanza, amenusurika Kubakwa na Mwajiri wake alietaka kufanya nae Mapenzi kwa nguvu.


Akizungumzia tukio hilo, binti huyo ambae ni mhitimu wa darasa la saba mwaka 2012 amesema kuwa Siku ya Jumamosi ya July 12 Mwaka huu, bosi wake alifika nyumbani siku hiyo akitokea disco ambapo yeye alikwenda Kumfungulia mlango na alipoingia ndani akaanza kumng’ang’aniza kufanya nae mapenzi.


Aliongeza kuwa Wakati tukio hilo linatokea Mama Mwenye nyumba ambae ni Mke wa mtuhumiwa huyo hakuwepo nyumbani, kwani alikuwa amesafiri kwenda kwao kusalimia Mkoani Arusha.


Binti huyo amebainisha kuwa mwajiri wake huyo (baba mwenye nyumba) alimng’ang’ania ili kufanya nae Mapenzi lakini alimkatalia kutokana na hofu aliyokuwa nayo huku akitumia juhudi mbalimbali kumshawishi kufanya nae mapenzi ikiwa ni pamoja na kumpatia pesa kiasi cha shilingi 10,000 kwa ajili ya kufanya nae mapenzi sanjari na kuficha siri hiyo.


Baada ya Mvutano huo, hatimae mwajiri wa Binti huyo (baba) alimwanchia ambapo binti huyo alimfuata binti mwingine mdogo waliekuwa wakikaa nae katika nyumba hiyo na kumuelezea tukio hilo, ambapo binti huyo alimshauri kumpigia simu mama mwenye nyumba kwa ajili ya kumpa taarifa hizo.


“Tulienda tukanunua Vocha ya 500 tukampigia mama siku hiyo hiyo ambapo baada ya kumpa hiyo taarifa kesho yake (jana) ndo mama mwenye nyumba akawa amefika nyumbani na kuniambia nikusanye nguo zangu ili mamdogo anifuate…”Alisema Binti huyo.


Mtuhumia anaetuhumiwa kutaka kufanya unyama huo ametajwa kwa jina la (----) Mkazi wa Igoma Jijini Mwanza, ambae ni Meneja wa Kanda ya Ziwa kutoka Kampuni ya (------).Majina yamehifadhiwa kwa muda ili kukamilisha uchunguzi wa Suala hili na hatimae kuwekwa bayana.



Binti alienusurika Kubakwa.

Mama mdogo wa Binti alietakwa kubakwa (Hakutaka Kuandikwa jiana lake) ambae ndiye aliempeleka binti huyo kwa ajili ya kufanya kazi za ndani nyumbani kwa Mtuhumiwa huyo, amesema kwamba binti huyo alimpigia simu jana (Jumapili) na kumpa taarifa hizo ambapo mapema leo (Jumatatu) ameenda nyumbani hapo na kumkuta mama mwenye nyumba ambae amekiri nae yeye kupokea taarifa za mfanyakazi wake kutaka kubakwa.





“Mimi alinipigia Simu jana jioni (Jumapili) nikiwa nyumbani sasa nikasema usiku huu siwezi kwenda kumfuata ikabidi nilale hadi asubuhi ambapo nimeenda leo (Jumatatu) asubuhi na kumkuta mama mwenye nyumba ambae nae alieza kusikitishwa na tabia ya mme wake kwa kuwa hiyo ni mara ya pili kuonyesha tabia ya aina hiyo kwa wafanyakazi wake wa ndani kwani hata mfanyakazi aliekuwepo awali nae aliondoka nyumbani hapo kutokana na tabia hiyo”.


“Nilivyofika nyumbani sikumkuta huyo mwanaume (Mtuhumiwa) na hata nilipompigia simu alipokea na kuanza kunifokea kuwa mimi niseme kama kuna kitu kingine ninachokitafuta kutoka kwake maana hayo mambo yameisha na tayari amemuomba msamaha (binti) hivyo kama kuna kitu kingine anachikitaka aseme badala ya kumfuatilia” alisema mama mdogo wa binti huyo baada ya kwenda kumfuata huyo binti.


Alipotafutwa mtuhumiwa huyo (Jina tunalo) kwa njia ya simu hii leo (Jumatatu) ili kuelezea juu ya tuhuma anazopewa hakuwa tayari kuzungumza badala yake alielekeza kuwa atafutwe mwanasheria wake ambapo alitoa namba za mwanasheria wake ambaye katika msg aliyotuma jina la Mwanasheria huyo liliandikwa “Makaza Advovate”.


Hatimae mwanasheria huyo alipigiwa simu na kujifanya hajui chochote juu ya tukio hilo na baada ya kuelezwa na mwandishi wa habari hizi kuwa taarifa hii ingeweza kutolewa bila upande wa pili kusikilizwa aliamua kukubali kukutana na mwandishi wa habari hii katika ofisi alizoziita za kwake japo hakukua na ishara yoyote ya kuonyesha kuwa ofisi hiyo ni ya wanasheria iliyoko katika jengo la ECKACLIF Isamilo Jijini Mwanza ghorofa ya pili.


Mwandishi wa habari hizi alipofika katika jengo hilo la ECKACLIF akiwa ameambata na mwenzake mmoja alikutana na mwanasheria huyo ambae alikuwa na mwenzake katika ofisi hiyo na katika kuelezea tukio hili yeye alisema kuwa ni bora mwandishi akaenda polisi kufungua mashtaka badala ya kupoteza muda jambo ambalo haliwezi kusaidia chochote.


Baada ya Mvutano mrefu baina ya mwandishi wa habari hizi, akiwa na mwenzake aliamua kutoka ndani ya ofisi hiyo ya mwanasheria wa Mtuhumiwa huyo bila kupata maelezo yoyote kutokana na tuhuma za tukio hizo, huku mtuhumiwa akibainisha kwa njia ya simu kwamba maelezo yaliyotelewa na mwanasheria wake ndiyo yako sahihi na hakuwa na cha ziada.


Busara za mwandishi ni kwamba vitendo hivi visipodhibitiwa katika jamii, tutaendelea kushuhudia watoto wetu wakipitia manyanyaso makubwa ya kiukatili katika jamii zetu. Hili suala sasa haliko chini ya Mwandishi tena bali yeye amelileta katika jamii kwa imani kwamba Wanaharakati wanahusika na utetezi wa Haki za Watoto, Haki za Wanawake ama Haki za Binadamu wanaweza kulifuatilia suala hili kwa kina zaidi.
USIKOSE KUFUATILIA CHAPISHO LIJALO JUU YA TAARIFA HII.
Na: Mwandishi wetu.

No comments:

Powered by Blogger.