Baada ya
kulifunga minyororo gari hilo, kama kawaida yao wakusanya Ushuru wa Maegesho
walisimama pembeni ya gari hilo ili kumsubiria mwenye gari na ndipo walipopigwa
na butwaa baada ya kubaini kuwa gari hilo lilikuwa la Mh.Wenje.
Pasipo
kujali sheria inasemaje kuhusiana na mtu anaekiuka sheria ya Maegesho, Watoza
ushuru hao walilifungua gari hilo bila kuonekana kumueleza Mh.Wenje jambo
lolote ikiwa ni pamoja na kumtaka kutoa faini kama ambavyo wamekuwa wakifanya
kwa watu wengine ambao wamekuwa wakikamatwa kwa kosa la kupaki katika maeneo
yasiyoruhusiwa, ambapo wamekuwa wakiwatoza faini hadi kiasi cha shilingi
50,000.
|
No comments: