LIVE STREAM ADS

Header Ads

HATMA YA WATUHUMIWA WA MAUAJI YA KAMANDA BARLOW BADO KITENDAWILI.


Aliekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza-Barlow
Kesi ya Mauwaji ya aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza Riberatus Barlow, imeendelea kusomwa katika Mahaka ya Hakimu Mkazi Mkoani Mwanza.
 
Kesi hiyo  ambayo inawakabiri watuhumiwa
saba inaendelea kupigwa tarehe kutokana na ushahidi wake kutokamilika mpaka sasa.

Watuhumiwa hao ni Muganyizi Maicco Peter (30) Mkazi wa Nyakabungo Mkoani Mwanza, Chacha Wekena Mwita (50) Mkazi wa Gongo la Mboto Jijini Dar es salaam, Magige Mwita Marwa (48) Mkazi wa Bugarika Mkoani Mwanza.

Wengine ni Mganzi Edward (22) Mkazi wa Tandika Jijini Dar es salaam, Bhoke Marwa Mwita (42) Mkazi wa Mombasa Ukonga, Andallah Petro (32) Mkazi wa Mji Mwema Mkoani Mwanza na Abdulhaman Ismail Athman (28) Mkazi wa Mkudi Mkoani Mwanza.

Hakimu Mkazi Angelous Rumishaba, alieleza kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na kesi namba 30 ya mwaka 2012 ya mauaji kinyume na kifungu  cha sheria 196 na 197 ya sheria ya kanuni za adhabu,sura ya 16 iliyofanyiwa marejesho mwaka 2002.

Alieleza kwamba washitakiwa hao walitenga kosa hilo la mauwaji usiku wa kuamkia Oktoba 13 mwaka 2012,katika eneo la kitangiri minazi mitatu wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza.

Kamanda Barlow aliuawa na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, mwaka 2012, majira ya saa nane usiku kwa kupigwa risasi shingoni, wakati akirejea nyumbani kwake akitoka katika kikao cha harusi ya binamu yake.
Kesi hiyo ilisomwa jumanne wiki hii na imeahirishwa tena hadi Septemba nne mwaka huu itakaposomwa tena.
Na Prisca Japhes: Mtanzania Media-Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.