LIVE STREAM ADS

Header Ads

USAILI SERENGETI DANCE LA FIESTA NA SERENGETI SUPER NYOTA NI LEO MKOANI MWANZA.



SERENGETI DANCE LA FIESTA:
Washriki lazima wawe kwenye kundi la kuanzia watu wanne mpaka nane, Na wawe na umri wa kuanzia miaka
18 na kuendelea, Kujiandikisha ni leo uwanja wa Nyamagana kuanzia saa kumi jioni mpaka saa kumi na mbili jioni, fainali za dance la Fiesta ni alkhamis ya wiki hii ya tarehe saba kuanzia saa tano asubui pale jembe ni jembe na mshindi atajishindia sh Milioni moja. 

SERENGETI SUPER NYOTA DIVAZ:
Hili ndo shindano lilitoa wasanii wengi wachanga ambao kwa sasa wamekuwa wakubwa na wamepata mafanikio, ambao wote wanatokea hapahapa Mwanza, Hapa unamzungumzia Young Killer aliyekuwa mshindi wa ujumla mwaka juzi pamoja na Mo Music aliyeishia nafasi ya tatu mwaka jana hapa mwanza wote hawa wanafanya vizuri kwa hivi sasa,

Kwa zaidi ya Miongo miwili Super Nyota ilikuwa ikitoa nafasi kwa jinsia zote mbili kushiriki yaani wavulana na wasichana, lakini mwaka huu tumebadili na kuamua kutoa nafasi kwa wasichana pekeake, ambae yoyote Yule ambae ni msichana na ana kipiaji ndo atapata nafasi kushiriki , ambapo mshindi atapelekwa Dar Es Salaam kwa ajili ya kushindanishwa na washiriki wengine toka katika Mikoa mingine.

Kujiandikisha ni leo uwanja wa Nyamagana kuanzia saa kumi jioni mpaka saa kumi na mbili jioni, fainali zake ni alhamis ya wiki hii ya tarehe saba kuanzia saa tano asubui pale jembe ni jembe na mshiriki lazima awe na umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea.

Kwa sasa Habari ya Mjini kwa Wapenda Burudani ni juu ya Show ya Serengeti Fiesta 2014 ambayo kwa mara ya Kwanza Mwaka huu Utepe utakatwa katika Jiji la Mwanza ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba. Wengi walikuwa wakijiuliza ni Wasanii gani watapanda katika Jukwaa la Serengeti Fiesta 2014 Jijini Mwanza. 

Sasa Mtanzania Media inakupa Mtonyo Mzima kuhusiana na List hiyo ya wasanii watakaopafomu katika Show hiyo. Kumbuka Kiingilio ni Shilingi 5,000 tu. Kumbuka pia kwamba kile kinyang'anyilo cha Super nyota Mkoani Mwanza Mwaka huu watapanda Jukwaani wasanii wa Kike Tu.Je nani ataibuka Super Nyota kwa wasanii wa Kike kutoka Mwanza? Jibu litapatikana siku hiyo ya tarehe 09.08.2014.
 
Hii ndiyo list yenyewe; Mkubwa na Wanawe, Young Killer, Ney wa Mitego, Linah, Mr.Blue, Makomandoo, Madee, Young Dee, Super Nyota, Vanessa Mdee, K-Style, Stamna, Baraka da Prince, Chege & Temba, Skylite Band, Mo-Music na Rais wa Wasafi Diamond Platnum.

SIKILIZA LIST NZIMA YA WASANII HAPA CHINI:

CHECK RATIBA NZIMA YA SERENGETI FIESTA 2014 KANDA YA ZIWA HAPA CHINI
Na Mhariri: Mtanzania Media.

No comments:

Powered by Blogger.