Pia walibainisha kuwa rushwa ya ngono ambayo
wamekuwa wakiombwa na baadhi ya maaskari imekithiri mitaani pindi wanapokamatwa
nyakati za usiku, jambo ambalo walisema limekuwa likiwaathiri kwa kuwa hadi
sasa baadhi yao wameambukizwa magongwa ya ngono ikiwemo virusi vya Ukimwi
sanjari na kupatiwa mimba jambo ambalo linazidi kuongeza idadi ya watoto
wanaoishi mitaani.
Akijibu Malalamiko ya Wasichana hao
kwa niaba ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Nyamagana, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi
ASP. Namsemba Mwakatobe amekiri kuwa malalamiko yanwasichana hao yanaweza kuwa
ni ya kweli ama laa, hivyo jeshi la polisi litahitaji ushirikiano wao kwa ajili
ya kuwabaini askari wake ambao wanakiuka maadili ya kazi yao kwa ajili ya
kuwachukulia hatua za kinidhamu.
|
No comments: