LIVE STREAM ADS

Header Ads

HII NI FAIDA NYINGINE YA DARAJA LA MABATINI JIJINI MWANZA.



Taswira ya daraja la Mabatini.Hii ilikuwa Mapema wakati ujenzi ukiendelea.
Baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wamesema kuwa pamoja na daraja la mabatini kuwa
msaada mkubwa kwao utokana na kupunguza ajali zilizokuwa zikitokea mara kwa mara katika eneo la Mabatini, pia daraja hilo limekuwa ni sehemu ya ajira kwao hususani kwa vijana wanaojishughulisha na shughuli ya upigaji picha.


Baadhi ya vijana wanaopiga picha katika eneo hilo wameleza kuwa, uwepo wa daraja hilo umeleta ahueni kwao na hivyo daraja hilo kutokana na daraja hilo kuwa sehemu mojawapo ya kujipatia kipato halali.


Jumanne Mbase ambaye ni mmoja wa wapigapicha katika daraja hilo alieleza kuwa, baada ya kuona daraja limekamilika, aliamua kuanzisha shughuli zake katika eneo hilo jambo ambalo lilimwongezea kipato zaidi tofauti na alivyokuwa hapo awali.


“Nilianza kazi hii darajani hapa mwezi wa  Machi  mwaka huu na kazi inaenda vizuri kwani kipato cha chini ninachopata kwa siku ni shilingi 5000 na siku kazi ikienda vizuri Napata shilingi elfu kumi hadi elfu kumi na mbili kwa siku..” Alieleza Jumanne.


Nae Jackson Jovin alieleza kwamba pamoja na wao kujiajiri mahali hapo, pia wamekuwa ni msaada katika kuhakikisha eneo hilo linakuwa salama wakati wote kwani  kwa uwepo wao hapo wamekuwa wakililinda eneo hilo  kwa namna moja  ama nyingine.


“Hatukai hapa kwa kupiga picha tu, bali tunaangalia usalama wa eneo hili kwa ujumla, wakati mwingine walinzi wanakuwa wamekaa huko chini na sisi tunapokuwa huku juu tunabeba jukumu la kuangalia usalama wa daraja hili.


Walieleza kuwa wapo baadhi ya watu ambao hufia katika daraja hilo na kutaka kufungua baadhi ya nati na wengine kukwangua kwa kutumi vitu vyenye ncha kali lakini wamekuwa wakidhibiti uharifu huo.


Wapigapicha wengine waliokuwa katika eneo hilo ambao ni Yohana Daud na Isack Musa walieleza kuwa , ni vema jamii ikatambua jinsi ya kujitafutia kipato, na sio kusubiri ajira kutoka serikalini huku wengine wakiishi amitaani kuvuta bangi.


Daraja hilo lilijengwa kutokana na eneo hilo kuwa na msongamano wa watu na magari, hivyo liliwekwa ili kupunguza ajari na vifo vilivyokuwa vikitokea mara kwa mara katika eneo hilo. 
Na Prisca Japhen-Mtanzania Media.

No comments:

Powered by Blogger.