LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAKAZI WA MBUGANI JIJINI MWANZA WATAKIWA KUTOTEGEMEA MISAADA.



Wakazi wa kata ya Mbugani  Jijini Mwanza wametakiwa kutotegemea misaada  kutoka serikalini, ili kukuza uchumi na  kuboresha rasilimali zilizopo kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.  

Akizungumza ofisini kwake
Mwenyekiti wa mtaa wa Mabatini Kaskazini kata ya Mbugani Ntobi Boniphas alisema kuwa wakazi wa maeneo hayo wanatakiwa kujituma katika shughuli mbalimbali ili kuleta maendeleo katika kata zao.

Alieleza kuwa zipo shughuli nyingi ambazo zinapaswa kufanywa na jamii husika bila kutegemea nguvu ya serikali wala msaada wowote  hususani katika utengezaji wa barabara za mitaa, ujenzi wa maabara na miradi mingine ya kimaendeeleo.

“ Tunatatizo la barabara kwa muda mrefu hali inayosababisha wananchi wakati wa mvua kushindwa kutoka majumbani kwenda katika shughuli zao za kila siku wakati uwezo wa kurekebisha barabara hizo tunao sisi kama jamii.”Alisema Boniphas.

Mwenyekiti huyo Pia katika kuhakikisha jamii inahusika kwa kila hali kuchangia maendeleo, alisema uongozi wa eneo hilo hutumia mikutano ya hadhara kuwahamasisha wananchi kujiletea maendeleo na kuzungumzia changamoto mbalimbali na jinsi ya kukabiliana nazo kama vile elimu, afya na miundombinu ya kata.

Pamoja na kuwepo na juhudi hizo za kuleta maendeleo ndani ya kata,Boniphas alieleza kwamba  hali ya ulinzi na usalama katika eneo hilo inaridhisha kutokana na kuwepo na ushirikiano na polisi jamii licha ya kuwa kila  mwananchi anajukumu la kulinda amani katika eneo lake analoishi. 

Hata hivyo amewataka wageni wanaoingia mtaani hapo kudumisha amani pia ushirikiano wanaoukuta ili kupunguza matukio ya kihalifu ambayo hapo awali yalikuwa mengi  katika baadhi ya mitaa. 
Na Prisca Japhes

No comments:

Powered by Blogger.