LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA USALAMA MTANDAONI.

Mtandao  wa kutetea  haki za   binadamu Tanzania (Tanzania   Human Rights  Denders  Coalition) (THRD) kwa kushirikiana  na   mtandao  wa kutetea  haki  za  binadamu   wa  Uganda   wameaandaa  kwa  mafunzo  ya  usalama  wa mtandaoni  kwa waandishi wa habari  wa Tanzania  ili  kuwapa  ujuzi wa kuzuia  taarifa  zao  kudukuliwa

Mafunzo  hayo  
yamewajumuisha  wadau   wa haki za habari  ambao ni waandishi wa habari, bloggers   na wafanyakazi  kwenye  sekta  ya  habari wapatao  kumi  na  nane  wakihudhuria   mafunzo  hato  katika  ukumbi wa  Regency  hotel  Jijini Mwanza.

Akifungua  mafunzo  hayo   mratibu wa   THRD   bwana  Onesmo  Ngurumo  alisema  kuwa  lengo  la mafunzo  hayo   ni kuwajengea  uwezo wa waandishi wa habari  wa  kulinda  taarifa  zao   hasa  kwenye  kuandika   habari za  uchunguzi  kuelekea  uchaguzi  mkuu wa mwaka 2015.

Ngurumo  aliwataka    washiriki  wote  kuzingatia  mafunzo  hayo kwa umakini  kwa kuwa  kwa sasa   suala  la  kudukuliwa  kwa   taarifa limezidi kuongeza, lakini  kwa kutumia  mafunzo  hayo  waandishi wataweza kulinda  taarifa  zao  kwa umakini    kwa kutumia  mbinu  mbalimbali zitakazotumika.

Ngurumo    alisema kuwa  usalama wa mtandaoni kwa   waandishi wa habari  ni muhimu  sana  kwani  kwa sasa  watawala wengi  hawapendi matumzi ya   mitandao ya kijamii  kutokana  na  kuhisi kuwa    inawachafua  na kuharibu  mifumo  yao  ya  kiutawala.

Naye  mwezeshaji  wa  mafunzo hayo toka  Uganda  bwana  John Kaoneka   alisema  kuwa  suala  la  udukuzi   duniani  limekuwa  kubwa  sana  kiasi  cha  kulalamikiwa  na  Nchi  mbalimbali, hivyo  kuna  kila sababu  ya   kila mtumiaji wa  mtandao  wakiwemo waandishi  wa habari kufahamu   kwa kina njia  za kupambana  na  udukuzi  ili  kubabiliana  na  changamoto  hiyo.

Naye  mshiriki  wa mafunzo  hayo  bwana  Josephat  Isango  Ngimba  alisema kuwa  mafunzo  hayo  yatamsaidia kwa kiasi kikubwa  cha  kutumia mifumo  mbalimbali  ya kulinda taaarifa  zake kwenye  kompyuta  yake.
Na:Edwin Soko-Dar es salaam

No comments:

Powered by Blogger.