LIVE STREAM ADS

Header Ads

HAPPY BIRTH DAY GB AMBAE NI C.E.O WA BINAGI MEDIA GROUP NA STAFF WA METRO FM.

George Marwa Binagi-GB Pazzo.
Ilikuwa ni February 26 Miaka kadhaa iliyopita, Mtoto George Marwa Binagi, GB Pazzo kama ninavyojulikana zaidi kwa hivi sasa niliweza kuzaliwa ambapo kuzaliwa kwangu kulitokana na Ushirikiano mzuri kati ya Wazazi wangu wapendwa The Late Mzee Daniel Marwa Binagi pamoja na Leah Daniel Binagi.

Hakika ni jambo jema kuona kwamba pamoja na changamoto zote katika uso wa dunia hii, bado Mola anazidi kunitazama kwa jicho la pekee na hatimae leo alhamisi February 26, 2015 nimeongeza idadi ya miaka tangu kuzaliwa kwangu.

Japo bado safari ni ndefu lakini mimi nasema kwamba haikuwa kazi rahisi hadi kufikia hatua niliyoifikia hivi sasa katika kuelekea kwenye mafanikio yangu, bali ni kwa rehema na Uweza wa Roho Mtakatifu.

Hakika sitawasahau ndugu, jamaa na marafiki wote ambao kwa namna moja ama nyingine waliweza kufanyika msaada mkubwa kwangu na hatimae hii leo nimefika hapa nilipo. Yapo mengi ambayo yametendeka. Mengi mazuri na machache mabaya. Sina neno la kusema zaidi ya MNISAMEHE PALE NILIPOWAKWAZA. Kwa upande wangu moyo wangu ni mweupe na hakuna hata mmoja nilie na kinyongo nae. Hakika Mwenyezi Mungu azidi kutuongoza vyema.

Yapo mengi sana ya kusema ila najua nikiyasema yataiondoa furaha niliyonayo siku ya leo, hivyo sina budi kuyaacha. Nikiwa Mtangazaji na Mwandishi wa Habari ninaefanya kazi na 99.4 Radio Metro Fm, Mwanza na C.E.O wa Binagi Media Group, nina imani kwamba siku zote jamii inayonizunguka itaendelea kunufaika na kazi zangu huku nikilenga zaidi kuchochea uelewa na mabadiliko ya kimaendeleo kwa kila mmoja.


NIMEJIFUNZA KWAMBA HAKUNA MAFANIKIO BILA CHANGAMOTO HIVYO TUSIKATE TAMAA PALE TUNAPOKUMBANA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI. JAMBO PEKEE NINALOWEZA KUTAMATISHA NALO NI KWAMBA “MTU AKIWA NDANI YA KRISTO, AMEKUWA KIUMBE KIPYA, YA KALE YOTE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA”. 2 WAKORINTHO 5:17.
"HAPPY BIRTH DAY TO MYSELF".

No comments:

Powered by Blogger.