LIVE STREAM ADS

Header Ads

WANAOFADHIRI UTEKAJI WA WATU WENYE ULEMAVU WA NGOZI WATAJWA.

Kulia ni Peter Ash ambae ni Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea haki za watu wenye ulemavu wa ngozi Under The Same Sun lenye Makao yake Makuu nchini Canada. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika hilo nchini Tanzania Vicky Mtetema.
Kufuatia Vitendo vya Utekaji na Maua kwa Watu wenye Ulemavu wa ngozi kuendelea kushamiri hapa nchini, Watu wanaodhaniwa kufadhiri vitendo hivyo wamefichuliwa ambapo Serikali imetakiwa kuwachulia hatua mara moja badala ya kuishia kusema hakuna Ushahidi wa Kutosha.

Akizungumza hivi Karibuni Jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Shirika la Kutetea haki za Watu wenye Ulemavu wa Ngozi Under The Same Sun lenye Makao yake Makuu nchini Canada Peter Ashi, alisema kuwa viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi vinauzwa kwa thamani kubwa hivyo wananchi wa kawaida hawawezi kumudu kuvinunua.

Kutokana na hali hiyo Ash aliwatupia lawama Wanasiasa kwa kuhusika moja kwa moja na vitendo hivyo vya kufadhiri Utekaji na Mauaji ya watu wenye Ulemavu wa ngozi hapa nchinini huku akiongeza kuwa mbali na baadhi ya watu waliowahi kukamatwa kwa kujihusisha na utekaji na mauaji ya Watu wenye ulemavu wa ngozi pia ongezeko la vitendo hivyo katika kipindi cha chaguzi hapa nchini vinaashiria kwamba baadhi ya wanasiasa wanajihusisha moja kwa moja na ufadhiri wa vitendo hivyo vya utekaji na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Ash aliyazungumza hayo huku akilaani tukio lililotokea disemba 27 mwaka jana ambapo mtoto ambae ni mlemavu wa ngozi Pendo Emmanuel (4) mkazi wa Kijiji cha ndami Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza kutekwa nyumbani kwao akiwa na wazazi wake ambapo mpaka sasa mtoto huyo hajaweza kupatikana licha ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo kutoa siku tano mtoto huyo awe amepatikana aidha akiwa hai ama mfu.

Wakati tukio hilo likiwaaacha watu wenye ulemavu wa ngozi wasijue la kufanya kutokana na maisha yao kuwa katika hali ya wasiwasi, mtoto Yohana Bahati (1) mkazi wa Kijiji cha Ilelema Wilaya ya Chato Mkoani Geita juzi January 15 majira ya saa mbili usiku pia ametekwa akiwa mikononi mwa mama yake mzazi huku watekaji hao wakimjeruhi mama yake Esther Bahati (30) wakati akipambana katika kumuokoa mwanae. Mama huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando na hali yake inaelewa kuwa mbaya kiasi cha kumfanya ashindwe kuongea baada ya kujeruhiwa kwa mapanga katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Bado juhudi za jeshi la polisi hapa nchini katika kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi hazijaweza kuzaa matunda ambapo juhudi zaidi zinahimizwa kuongezeka huku ndugu, jamaa na marafiki wakitakiwa kuongeza ushirikiano wao katika kuyanusuru maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi kutokana na unyanyasaji, utekaji na hata mauaji.

Sanjari na nayo, pia onyo lililotolewa hivi karibu na Serikali juu ya kuwapiga marufuku waganga wa kienyeji kujihusisha na vitendo vya ramli limetakiwa kutekelezwa ipasavyo kutokana na shuhuda mbalimbali kuonyesha kwamba matukio mengi ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi huchochewa vitendo vya lamri ambavyo vimekuwa vikifanywa na waganga wa kienyeji kwa kuwatabiria wateja wao kupeleka viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi kwa minajiri ya kuwapatia utajiri ama kuwafanikishia masuala yao mbalimbali jambo ambalo si sahihi.


Wakizungumza na Binagi Media Binagi baadhi ya watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja na ndugu, jamaa na rafiki zao wameishauri Serikali kutenga maeneo maalumu hapa nchini kwa lengo la kuwaweka watu wenye ulemavu wa ngozi pamoja ikiwa ni pamoja na kupatiwa huduma muhimu kama vile elimu, afya sanjari na ulinzi imara katika maeneo hayo.
Na: George Binagi-GB Pazzo

No comments:

Powered by Blogger.