OJADACT: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA SHERIA YA MAUDHUI YA UTANGAZAJI NCHINI.
Mkutano na waandishi wa habari….19/8/2015 10:30 Asb.. Uchambuzi wa sheria ya
maudhui ya utangazaji kuelekea uchaguzi
mkuu wa oktoba 25, 2015
Chama cha
waandishi wa habari wa
kupiga vita matumizi
ya dawa za kulevya na uhalifu tanzania (ojadact) kinachukua nafasi
hii kuongea nanyi waandishi wa
habari juu ya sheria ya
maudhui ya utangazaji ( the broadcasting
services content .
Ndugu waandishi wa
habari tunaelewa kuwa, mamlaka ya
utangazaji tanzania (tcra) ni chombo
kilichoundwa kisheria na kina wajibu wa kusimamia sekta
ya utangazaji nchini kama jinsi sheria no 12 ya mwaka 2003
iliyounda chombo hicho.
Kwa masikitiko makubwa tunawaambia
ndugu waandishi wa habari
kuwa sheria ilitangazwa kwenye
gazeti la serikali Juni 26,
2015 na kuanza kutumika .
Sheria hii imekuwa ni kitanzi kikubwa kwa tasnia ya habari nchini kwani inanyima uhuru wa vyombo vya habari(M&F) na Haki ya
kupata habari(RTI) wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 25
mwaka huu kama zilivyo sheria za makosa ya kimtandao na takwimu za mwaka 2015
pamoja na miswada ya
sheria ya haki ya kupata taarifa na ule wa huduma za vyombo vya habari ambayo ilizuiliwa kujadiliwa bungeni mwezi Juni, 2015.
OJADACT tumeitazama sheria ya maudhui ya utangazaji na kuona mapungufu yafuatayo…
·Sheria hii haijahusisha wadau wa habari na kwa namna moja au
nyingine inakosa Baraka za wadau jambo linalotia shaka
na kuwa kati ya
sheria za zinazotungwa kwa lengo la kukomoa kundi
fulani la kitaaluma.
·Sheria hiyo ina mkizano mkubwa
na misingi ya kitaaluma ya tasnia ya habari, mfano kutotambua falsafa ya vyombo vya habari na mlengo wao,kutotaka kutambua kuwa mtu
anaweza kutengeneza habari(Prominence), kudumaza uwezo wa Mwandishi kwenye mahojiano kwa kutofanya majadiliano mafupi
ya hitimisho na uchambuzi wa hoja za wahojiwa mwishoni mwa kipindi
· Sheria hii ina
imejichanganya katika utambulisho
wa vifungu vya kwanza na
maudhui ya kifungu
hivyo.(Rejea sehemu ya III kifungu cha 15 ) sehemu ya No
broadcast on poling day na tazama kifungu cha
maudhui cha 15.
·Sheria imeweka mitego mipana na
maana ya mambo ambayo hayatakiwi,Mfano kifungu cha 15 (2) maneno yafuatayo.. No broadcast any politically – related matter which may reasonable upset the balance to be observed …… Hapo ni wazi kuna mkizano wa maana pana inayoweza kutafsiriwa na mamlaka moja
tu yani watunga sheria na sio watumiaji wa sheria.
·Sheria pia imenyakua miongozo ya kitaaluma kwa mwandishi na
kuifanya sheria badala kuiacha katika maadili ya kitaaluma (Media ethics) ambayo ingeweza kusimamiwa na vyombo husika kama MCT, UTPC, OJADACT, MISA, TAMWANA na vingine. Rejea msisitizo wa sehemu ya II kifungu cha 4(a) – (i)
RAI:
·Kuwe na maridhiano ya pamoja baina ya TCRA na wadau wa habari ili kutazama utekelezaji wa sheria hii ili kutominya uhuru wa vyombo vya habari na haki ya kupata taaifa kwa wananchi.
·Serikali iache kuwa na ajenda ya siri
katika kuvibana vyombo
vya habari wakati huu
wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu badala
yake ishirikiane na
vyombo hivyo kutengeneza
ajenda ya kuwavusha
watanzania salama kwenye uchaguzi
huu.
·Wamiliki wa vyombo vya habari na
waandishi wa habari wawe makini na sheria
hii
MSIMAMO WA CHAMA
Sheria hii siyo rafiki kwa vyombo vya habari na inalenga kuvibana vyombo hivyo kutofanya kazi iapasavyo kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba, 25 mwaka huu,1-g kama zilivyosheria za makosa
ya mtandaoni na takwimu zinazoanza
kutumika mwezi Septemba 1, mwaka huu
ina ile miswada miwili ya haki ya kupata
taarifa na huduma
kwa vyombo vya
habari.
Imetolewa na;
Edwin
Soko
Mwenyekiti
OJADACT
19.08.2015
No comments: