LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANDISHI WA HABARI SALMA SAID APATIKANA BAADA YA KUTEKWA NA WATU WASIOJULIKANA.

Mwandishi wa habari Salma Said.
Na George Binagi-GB Pazzo kwa Msaada wa Mtandao.
Mwandishi wa Habari wa Idhaa wa Kiswahili ya Ujerumani ya DW (Deutsche Welle) anaewakilisha Visiwani Zanzibar, Salma Said, amepatikana baada ya kutekwa na watu wasiojulikana ijumaa iliyopita.

Jana jioni Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Simon Siro alithibitisha kupatikana kwa mwandishi huyo, alietekwa akiwa katika uwanja wa Mwalimu Julias Nyerere Jijini Dar es salaam.

Pia mmewe Salma Said, Ali Salim Khamis amethibitisha kupatakana kwa mkewe na taarifa za awali zinaeleza kuwa Salma hajapatikana na majeraha wala madhara yoyote kutokana na utekaji huo.

Haijulikani Salma alitweka kwa minajiri ipi na wahusika ni akina nani, japo kutekwa kwake kumehusishwa na kazi yake ya uandishi wa habari ambayo pia huifanya katika magazeti kadhaa hapa nchini na kwamba huenda utekaji huo ulidhamiria kumkwamisha asiripoti habari za Uchaguzi Mkuu wa Marudio Visiwani Zanzibar uliofanyika jana Machi 20.

Binagi Blog inalaani utekaji huo si tu kwa kuwa alietekwa ni mwana habari, bali kwa raia yeyote katika ardhi ya Tanzania kwa kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na ukiukwaji wa Haki za Binadamu.
Bonyeza HAPA na HAPA Kwa Matamko Kadhaa.

No comments:

Powered by Blogger.