LIVE STREAM ADS

Header Ads

Ujumbe kutoka USAID Marekani waipongeza Tanzania.

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.

Binagi Media Group
Mapambano dhidi ya ugongwa hatari wa Malaria yameendelea kuonyesha mafanikio mkoani Mwanza, baada ya vifo vitokanavyo na ugonjwa huo kupungua kutoka asilimia 19.01 mwaka 2011/12 hadi asilimia 15.1 mwaka 2015/16.

Hiyo ni kutokana na juhudi za serikali kupambana na ugonjwa huo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa USAID ambalo limeendelea kusaidia vyandarua vyenye kinga kwa ajili ya mapambano dhidi ya malaria.

Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonard Subi aliyasema hayo jana wakati wa zoezi la kugawa vyandarua bure katika shule ya msingi Sese iliyopo Kata ya Bujashi wilayani Magu ambalo lilishuhudiwa pia na ujumbe kutoka USAID Marekani.

Alisema mbali na kuua vimelea vya Malaria kwa kutumia viuatilifu, pia serikali inagawa vyandarua bure katika shule za msingi, vituo vya afya, zahanati pamoja na hospitali ili kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Monica Ngalula pamoja na Marco Yusuph ni baadhi ya wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Sese, walishukuru kwa kugawiwa vyandarua hivyo na kwamba vitawasaidia wasing’atwe na mbu wa Malaria wakiwa wamelala nyumbani kama ilivyokuwa hapo awali.


Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka USAID, Chriss Thomas alifurahishwa na juhudi za Tanzania kupambana na ugonjwa wa Malaria na kuahidi ushirikiano zaidi wa kusaidia mapambano hayo ili kuokoa maisha ya watu hususani akina mama wajawazito pamoja na watoto ambao wamekuwa kwenye hatari ya kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo.

Mganga Mkuu mkoani Mwanza, Dkt.Leonard Subi
Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka USAID, Chriss Thomas akizungumza na wanahabari
Ujumbe kutoka USAID Marekani ukiwa shule ya msingi Sese wilayani Magu kushuhudia zoezi la ugawaji vyandarua
Mwanafunzi wa shule ya msingi Sese akipokea chandarua kutoka USAID
Mwanafunzi wa shule ya msingi Sese akipokea chandarua kutoka USAID
Ugeni kutoka USAID Marekani
Shule ya msingi Sese wilayani Magu ni miongoni mwa shule za msingi 941 ambazo wanafunzi wake wananufaika na zoezi la ugawaji vyandarua bure mkoani Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.